wakili wake wa utetezi, Hudson Ndusyepo leo katika mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu jijini Dar es Salaam kabla ya upande wa utetezi wake kuuliza maswali upande wa Mashtaka.
Na Karama Kenyunko, Blogu ya jamii.
Mahakama
ya Hakimu Mkazi Kisutu, siku ya ijumaa itatoa maamuzi dhidi ya kesi ya
matumizi ya dawa za kulevya inayomkabili mfanyabiashara maarufu nchini
Yusuph Manji kama ana kesi ya kujibu ama la.Hakimu
Mkazi Mfawidhi, Cyprian Mkeha amesema hayo leo mapema baada ya upande
wa mashtaka kufunga ushahidi dhidi ya kesi hiyo kwa kuita mashahidi
watatu.
Kabla
ya uamuzi huo kutolewa, shahidi wa tatu na wa mwisho, Mkemia kutoka
Ofisi ya Mkemia Mkuu wa Serikali, Domician Dominic (49) ameshindwa
kuithibitishia mahakama hiyo kama sampuli ya mkojo alioufanyia uchunguzi
ni wa Mfanyabiashara Yusufu Manji au Polisi.
Akijibu
swali wakili wa utetezi, Hudson Ndusyepo la kumtaka, kuieleza mahakama
kama anatambua mkojo huo ni wa nani alisema, hatambui kama mkojo ni wa
Manji au Polisi kwa kuwa hakuwepo msalani wakati sampuli hiyo inatolewa
badala yake yeye alitoa kontena na kumpatia Polisi ili Manji aweke
sampuli hiyo ambapo baada ya kuipokea Kutoka kqa Koplo Sospeter.
Alisajili kontena hilo kwa kuipa namba ya maabara 367/2017.
Ameongeza katika uchunguzi wa awali aliofanya aligundua mkojo huo ulikuwa na kemikali inayoitwa benzodiazepines.
Akiongozwa
na Wakili wa Serikali, Timon Vitalis, Shahidi huyo amedai mahakamani
hapo kuwa kemikali zilizokutwa kwenye mkojo Wa Manji ni dawa ambao
hutumika kwa ajili ya kupunguza maumivu makali kwa maelekezo ya daktari
na pia kumsaidia mgonjwa kupata usingizi.
Ameongeza,
katika hatua ya pili ya uchunguzi aligundua dawa inayoitwa Morphine
yenye viashiria vya heroine ambayo wakati mwingine hutumika wakati wa
upasuaji.
Mfanyabiashara maarufu nchini, Yusuph Manji akizungumza na
wakili wake wa utetezi, Hudson Ndusyepo leo katika mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu jijini Dar es Salaam kabla ya upande wa utetezi wake kuuliza maswali upande wa Mashtaka.
Mfanyabiashara maarufu nchini, Yusuph Manji akielekea kupanda Gari akielekea Mahabusu. Agosti 25 mwaka huu ambayo ni Ijumaa Uamuzi kama ana kesi ya kujibu au la katika kesi ya dawa za kulevya kujulikana rasmi.
Picha na Avila Kakingo, Globu ya Jamii.
Mfanyabiashara maarufu nchini, Yusuph Manji akizungumza na
wakili wake wa utetezi, Hudson Ndusyepo leo katika mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu jijini Dar es Salaam kabla ya upande wa utetezi wake kuuliza maswali upande wa Mashtaka.
Mfanyabiashara maarufu nchini, Yusuph Manji akielekea kupanda Gari akielekea Mahabusu. Agosti 25 mwaka huu ambayo ni Ijumaa Uamuzi kama ana kesi ya kujibu au la katika kesi ya dawa za kulevya kujulikana rasmi.
Picha na Avila Kakingo, Globu ya Jamii.
No comments:
Post a Comment