Kampuni ya Simu Tanzania TTCL imezindua huduma ya teknolojia mpya
ya 4G LTE mkoani Iringa ili kuongeza kasi ya maendeleo na kuimarisha
mawasiliano katika mkoa huo.
Hafla hiyo ya uzinduzi ilihudhuriwa na Mgeni Rasmi, Mkuu wa Wilaya ya
Kilolo, Asia Abdallah aliyemuwakilisha Mkuu wa Mkoa wa Iringa, Amina Masenza,
Mkuu wa Wilaya Iringa, Richard Kasesera, Afisa Mtendaji Mkuu wa
TTCL, Waziri Kindamba, Mbunge wa Iringa Mjini, Mchungaji Peter
Msigwa na Meneja wa TTCL –Iringa, Mhandisi Ekael Manase.
Akizindua huduma hiyo Mgeni rasmi alisema Mkoa wa Iringa ni maarufu
kwa mazao ya kilimo na biashara hivyo huduma hiyo itawanufaisha
wananchi kuwasiliana na kupeana taarifa kuhusu shughuli mbalimbali za
maendeleo.
Aidha amesema kuanzishwa kwa huduma hiyo mkoani humo ni fursa
nyingine kwa wananchi kwani itatoa mchango mkubwa katika sekta
mbalimbali ikiwemo elimu, afya, usafiri, biashara, utalii, huduma za jamii na
sekta nyingine mbalimbali.
“Natumia fursa hii kutoa rai kwa Wana Iringa na Wananchi kwa ujumla
kutumia TTCL kwani ni Mtandao wa wenye huduma bora na tozo nafuu,
zenye kukidhi mahitaji ya Makundi yote katika jamii” Alisema Mkuu wa
Wilaya ya Kilolo kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Iringa, Dc Asia
Abdallah.
Aidha, mgeni rasmi amewataka Wakazi wa Iringa kuziona fursa za
kibiashara zinazotolewa na TTCL kama vile kuwa Wakala wa kuuza vocha,
wakala wa TTCL PESA na huduma mbalimbali zitolewazo na kampuni hii ili
waweze kujipatia kipato.
Katika hatua nyingine alitoa changamoto kwa TTCL kupanua wigo wa
huduma zake ili kuyafikia maeneo ya vijijini ambako zinafanyika shughuli
nyingi za kiuchumi hasa Kilimo na biashara ambavyo vinahitaji sana
Mawasiliano ya uhakika.
Naye, Afisa Mtendaji Mkuu wa TTCL, Waziri Kindamba aliwataka
wananchi kutumia huduma za TTCKL ambazo zimeboreshwa zaidi ili
kukidhi mahitaji ya wateja wetu.
“Uzinduzi wa huduma hiyo, ni utekelezaji wa mpango mkakati ambao TTCL
imejiwekea kwa kusambaza huduma za mawasiliano bora nchini kote.
Uzinduzi wa huduma ya 4G, ni miongoni mwa hatua za utekelezaji wa
mpango mkakati huo, ambao unaongeza idadi ya mikoa iliyofikiwa kuwa 15
kati yake 13 ya Tanzania Bara na miwili ya Tanzania visiwani ”amesema
Bw. Waziri Kindamba.
Aidha, Afisa Mtendaji Mkuu aliwahakikishia wananchi kuwa TTCL
imejipanga vyema katika kuhakikisha inatoa huduma bora ya mawasiliano
ya simu ya Mkononi, mezani na huduma bira ya Intaneti.
Mkuu wa Wilaya ya Kilolo, Asia Abdallah kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa Iringa, Amina Masenza (wa tatu kulia), akiwa ameshika bango sambamba na Afisa Mtendaji Mkuu wa TTCL, Waziri Kindamba (wa pili kushoto) pamoja na Mbunge wa Iringa Mjini, Mchunaji Peter Msingwa (kushoto), wakiashiria uzinduzi wa huduma ya TTCL 4G mkoani Iringa
na kushuhudiwa na Mkuu wa Wilaya Iringa, Richard Kasesera (wa pili kulia) pamoja na Meneja wa TTCL Mkoa wa Iringa, Mhandisi
Ekael Manase.
Afisa Mtendaji Mkuu wa TTCL, Waziri Kindamba (katikati) akimuonesha matumizi ya Simu ya Mezani isiyotumia waya, Mkuu wa Wilaya ya Kilolo, Asia Juma Abdallah katika uzinduzi wa huduma ya 4G mkoani Iringa.
Afisa Mtendaji Mkuu Bw.Waziri Kindamba akimuonesha Mbunge wa Iringa
Mjini, Mchunaji Peter Msingwa jinsi huduma ya 4G ilivyobora na spidi
kubwa ya Intaneti, katika hafla ya uzinduzi wa 4G Iringa.
Afisa Mtendaji Mkuu wa TTCL, Waziri Kindamba akihutubia kwenye hafla ua
uzinduzi wa huduma ya TTCL 4G Mkoani Iringa.
Afisa Mtendaji Mkuu wa TTCL, Waziri Kindamba (wa pili kushoto) akimuonyesha Mkuu wa Wilaya ya Kilolo, Asia Juma Abdallah namna huduma hiyo inavyofanya kazi wakati wa huduma ya 4G mkoani Iringa. Wengine pichani toka kushoto ni Mbunge wa Iringa Mjini, Mchunaji Peter Msingwa, Mkuu wa Wilaya Iringa, Richard Kasesera (wa pili kulia) pamoja na Meneja wa TTCL Mkoa wa Iringa, Mhandisi Ekael Manase.
No comments:
Post a Comment