HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Wednesday, August 30, 2017

SERIKALI YAWEKA MIKAKATI YA MICHEZO KATIKA MASHINDANO MBALIMBALI.

Na Chalila Kibuda, Globu ya Jamii.
SERIKALI imejipanga katika masuala ya michezo  kutoa nguvu pamoja na kuenzi michezo ya shule za misingi na Sekondari ili kuweza kushiriki mashindano mbalimbali ya Kikanda na Dunia na wachezaji kurudi medali za dhahabu.

 Hayo ameyasema leo Waziri Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Dk Harrison Mwakyembe wakati akipokea bendera ya Taifa kwa wanafunzi wa Shule ya Sekondari Makongo ambao walishiriki mashindao ya Shule za Sekondari za Jumuiya ya Afrika Mashariki yaliyofanyika Uganda (FEASSSA) hivi karibuni, amesema wanafunzi wameonesha vipaji na kuweza kushika na nafasi ya tatu katika mashindano hayo.

Amesema kuwa shule zilizoshiriki zimeweza kutangaza Tanzania hivyo katika mashindano yajayo nguvu itaongezeka  kwa sekondari nyingi kushiriki na kasha kuweza kupata wachezaji mbalimbali ikiwemo timu ya taifa pamoja na riadha.

Dk. Mwakyembe amesema kuwa katika Wizara hiyo atahakikisha wanafnaya vizuri katika michezo kwa kuweza kupata ushindi  ikiwa kwa vilabu vyote vya michezo kujipanga.
Amesema katika michezo hakuna uchawi kinachohitajika ni juhudi na maarifa kwa wachezaji wanavyoshiriki mashindano yeyote ya ndani na ya nje ya nchi.

Aidha amesema wanafunzi walioshiriki na kushika nafasi ya tatu waongeze juhudi katika mashindano yajayo waweze kuwa washindi wa kwanza katika mashindano ya (FEASSSA).

 Waziri Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Dk Harrison Mwakyembe akizungumza baada ya kupokea Bendera kwa wanafunzi wa  Shule ya Makongo walioshiriki mashindao ya Shule za Sekondari za Jumuiya ya Afrika Mashariki yaliyofanyika Uganda (FEASSSA) leo jijini Dar es Salaam.
Waziri Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Dk Harrison Mwakyembe akimvisha medali mwanafunzi wa Shule ya  Sekondari Makongo, Winfrida Makenji aliyepata medali nne za mshindi wa tatu katika mashindao ya Shule za Sekondari za Jumuiya ya Afrika Mashariki yaliyofanyika Uganda (FEASSSA) leo jijini Dar es Salaam.
Waziri Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Dk Harrison Mwakyembe akipokea bendera kwa wanafunzi wa sekondari Makongo walioshiriki mashindao ya Shule za Sekondari za Jumuiya ya Afrika Mashariki yaliyofanyika Uganda (FEASSSA) leo jijini Dar es Salaam.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad