HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Friday, August 18, 2017

RAIS DK.SHEIN AFANYA ZIARA YA KIKAZI MKOA KUSINI UNGUJA

 Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi pia Makamu Mwenyekiti wa CCM Zanzibar Dk.Ali Mohamed Shein akikata utepe jana na kulifungua Tawi la CCM Kizimkazi Dimbani Wilaya ya Kusini Unguja wakati wa ziara yake katika Wilaya hiyo,(kushoto) Mwandawa Said Nassor.
  Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi pia Makamu Mwenyekiti wa CCM Zanzibar Dk.Ali Mohamed Shein alipokuwa akizungumza na WanaCCM wa Tawi la Kizimkazi Dimbani mara baada ya kulifungua Tawi hilo akiwa katika ziara katika Mkoa wa Kusini Unguja jana (kushoto) Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Kusini Unguja Bw.Ramadhan Abdalla Ali.
 Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein alipokuwa akifungua pazia kama ishara ya Uwekaji wa Jiwe la Msingi Ujenzi wa Nyumba ya Daktari katika Kijiji cha Muyuni "B" Wilaya ya Kusini Unguja alipofanya Ziara ya kutembelea Miradi ya Maendeleo katika Wilaya  hiyo jana.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein (kulia) akiwasalimia na wananchi  katika Kijiji cha Muyuni "B" Wilaya ya Kusini Unguja baada ya kuweka   Jiwe la Msingi Ujenzi wa Nyumba ya Daktari  katika kijiji hicho jana alipofanya Ziara ya kutembelea Miradi ya Maendeleo katika Wilaya   hiyo (Picha na Ikulu)

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad