HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Saturday, August 19, 2017

MWENYEKITI BARAZA LA TAIFA LA USALAMA BARABARANI, MHANDISI MASAUNI ATEMBELEA TEMESA NA CHUO CHA NIT, JIJINI DAR ES SALAAM LEO

Mwenyekiti wa Baraza la Taifa la Usalama Barabarani, ambaye pia ni Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni (katikati) akiwa na Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Ufundi na Umeme (TEMESA) Dkt. Mussa Mgwatu (kushoto) na Mkurugenzi wa Uzalishaji na Matengenezo Temesa, Mhandisi Sylvester Simfukwe (kulia), wakati Mwenyekiti huyo alipokuwa anatoka kuiangalia Karakana ya Utengenezaji wa Magari iliyopo katika ofisi za Temesa, Keko, jijini Dar es Salaam. Masauni alisema lengo kubwa la ziara yake, kuangalia jinsi gani Baraza lake linaweza kufanikisha Utekelezaji wa Mapendezo ya Kamati iliyoundwa na Baraza hilo ili kukabiliana ajali za barabarani nchini. Picha zote na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi.

Mwenyekiti wa Baraza la Taifa la Usalama Barabarani, ambaye pia ni Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni (aliyekaa), akimsikiliza rubani Edger Mcha (kulia) wa Chuo cha Usafirishaji nchini (NIT) kilichopo jijini Dar es Salaam, wakati alipokua anamuonyesha jinsi ya kuongoza ndege inapotaka kuruka na kutua kutoka katika kiwanja cha ndege. Mwenyekiti huyo alipata maelezo hayo wakati alipokua katika darasa la kufundishia marubani chuoni hapo. Masauni alifanya ziara katika chuo hicho na Wakala wa Ufundi na Umeme (TEMESA), kwa lengo la kuangalia jinsi gani Baraza lake linaweza kufanikisha Utekelezaji wa Mapendezo ya Kamati iliyoundwa na Baraza hilo ili kukabiliana ajali za barabarani nchini. Akiwa chuoni hapo aliangalia ukaguzi wa magari na pia kupata mipango mbalimbali waliyonayo kuhusiana na elimu wanayoitoa ya kuhusiana na usalama barabarani. Aliyevaa koti ni Mkuu wa Chuo hicho, ambaye pia ni Mjumbe wa Baraza hilo, Profesa Zakaria Mganilwa

Mwenyekiti wa Baraza la Taifa la Usalama Barabarani, ambaye pia ni Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni (kushoto) akiangalia mashine ya kukagua magari kwa njia ya umeme iliyokua inaonyeshwa na Mhandisi Yakubu wa Wakala wa Ufundi na Umeme (TEMESA. Katikati ni Meneja wa Karakana ya kutengeneza magari na mitambo mbalimbali ya Serikali, Julius Humbe. Masauni alifanya ziara katika ofisi hiyo iliyopo Keko, jijini Dar es Salaam, kwa lengo la kuangalia jinsi gani Baraza lake linaweza kufanikisha Utekelezaji wa Mapendezo ya Kamati iliyoundwa na Baraza hilo ili kukabiliana ajali za barabarani nchini

Mwenyekiti wa Baraza la Taifa la Usalama Barabarani, ambaye pia ni Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni akiiongoza ndege katika darasa la kufundishia marubani katika Chuo cha Usafirishaji nchini (NIT) kilichopo jijini Dar es Salaam. Masauni alifanya ziara chuoni hapo kwa lengo la kuangalia jinsi gani Baraza lake linaweza kufanikisha Utekelezaji wa Mapendezo ya Kamati iliyoundwa na Baraza hilo ili kukabiliana ajali za barabarani nchini. Akiwa chuoni hapo aliangalia ukaguzi wa magari na pia kupata mipango mbalimbali waliyonayo kuhusiana na elimu wanayoitoa hasa katika upande wa usalama barabarani. Kulia ni Mkuu wa Chuo hicho, ambaye pia ni Mjumbe wa Baraza hilo, Profesa Zakaria Mganilwa.

Mwenyekiti wa Baraza la Taifa la Usalama Barabarani, ambaye pia ni Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni (kushoto) akimsikiliza Mkuu wa Chuo cha Usafirishaji nchini (NIT), Profesa Zakaria Mganilwa (katikati) alipokua anatoa historia ya chuo hicho pamoja na kozi mbalimbali zinazofundishwa katika chuo hicho, kilichopo Mabibo jijini Dar es Salaam. Masauni alifanya ziara chuoni hapo kwa lengo la kuangalia jinsi gani Baraza lake linaweza kufanikisha Utekelezaji wa Mapendezo ya Kamati iliyoundwa na Baraza hilo ili kukabiliana ajali za barabarani nchini. Kulia ni Naibu Mkuu wa Chuo hicho kwa upande wa Taaluma Utafiti na Ushauri, Dk. Prosper Mgaya.

Mkuu wa Idara ya Teknolojia ya Usafirishaji wa Chuo cha Usafirishaji nchini (NIT), kilichopo Mabibo, jijini Dar es Salaam, Amon Mwasandube, akimuonyesha Mwenyekiti wa Baraza la Taifa la Usalama Barabarani, ambaye pia ni Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni (katikati), jinsi gari linavyokaguliwa linapokuja katika Kituo cha Ukaguzi wa Magari chuoni hapo. Masauni alifanya ziara chuoni hapo kwa lengo la kuangalia jinsi gani Baraza lake linaweza kufanikisha Utekelezaji wa Mapendezo ya Kamati iliyoundwa na Baraza hilo ili kukabiliana ajali za barabarani nchini. Kulia ni Mkuu wa Chuo hicho, Profesa Zakaria Mganilwa.
Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Ufundi na Umeme (TEMESA) Dkt. Mussa Mgwatu (kushoto), akimpokea Mwenyekiti wa Baraza la Taifa la Usalama Barabarani, ambaye pia ni Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni wakati Mwenyekiti huyo alipofanya ziara katika ofisi hizo zilizopo Keko Mwanga, jijini Dar es Salaam, kwa lengo la kuangalia jinsi gani Baraza lake linaweza kufanikisha Utekelezaji wa Mapendezo ya Kamati iliyoundwa na Baraza hilo ili kukabiliana ajali za barabarani nchini.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad