Na Karama Kenyunko,Glogu ya jamii.
MAHAKAMA
ya Hakimu Mkazi Kisutu leo mapema imeelezwa kuwa jalada la kesi ya
uhujumu uchumi dhidi ya aliyekiwa Mkurugenzi Mkuu Wa Vitambulisho vya
Taifa (Nida), Dickson Maimu, lipo kwa DPP.
Mwendesha Mashtaka, wakili wa serikali, Peter Vitalis ameeleza hayo mbelw ya Hakimu Mkazi Respicius Mwijage.
Amedai
kuwa shauri hilo leo lilikuja kwa ajili ya kutajwa lakini jalada halisi
la kesi hiyo liko kwa DPP na pia upelelezi bado haujakamilika, hivyo
likirejeshwa ndipo itafahamika upelelezi umefikia wapi.
Hata
hivyo, Hakimu Mwijage amesema kesi hiyo ina mwaka mmoja na upelelezi
haujakamilika, hivyo wakamilishe ambapo ameahirishwa kesi hadi
September 28/2017.
Katika
kesi hiyo, mshtakiwa Maimu na wenzake, wanakabiliwana mashtaka ya 27
yakiwemo ya kutumia madaraka vibaya, kula njama, kutumia nyaraka za
uongo kumdanganya mwajiri na kuisababishia Serikali hasara ya zaidi ya
Sh 1,169,352,931.
Mbali
ya Maimu, washtakiwa wengine Ni aliyekiwa Meneja Biashara Wa NIDA,
Avelin Momburi, Mkurugenzi wa TEHEMA, Joseph Makani. Kaimu Mhasibu Mkuu
wa NIDA, Benjamin Mwakatumbula, Mkurugenzi wa Kampuni ya Aste Insurance
Brokers, Astery Ndege, Ofisa Usafirishaji, George Ntalima, Mkurugenzi
wa Sheria, Sabina Raymond naXavery Kayombo.
No comments:
Post a Comment