HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Friday, August 25, 2017

IGP SIRRO AWASILI MKOA WA ARUSHA KWA ZIARA YA KIKAZI

Mkuu wa Jeshi la Polisi Nchini (IGP) Simon Sirro (kushoto), akisalimiana na Mkuu wa mkoa wa Arusha, Mrisho Gambo, wakati alipofika ofisini kwake kujitambulisha na kuzungumza na Wajumbe wa Kamati ya Ulinzi na Usalama ya mkoa huo tangu alipoteuliwa kuliongoza Jeshi hilo, IGP Sirro, yupo mkoani Arusha, kwa ziara ya kikazi ya siku mbili yenye lengo la kuzungumza na askari na maofisa wa Jeshi hilo pamoja na kujua changamoto wanazokutananazo wakati wanapotekeleza majukumu yao ya kulinda usalama wa raia na mali zao. Picha na Jeshi la Polisi.
Mkuu wa Jeshi la Polisi Nchini (IGP) Simon Sirro, akiwa katika picha na Mkuu wa mkoa wa Arusha, Mrisho Gambo, na baadhi ya wajumbe wa Kamati ya Ulinzi na Usalama ya mkoa huo wakati alipofika ofisini kwake kujitambulisha, , IGP Sirro, yupo mkoani humo, kwa ziara ya kikazi ya siku mbili yenye lengo la kuzungumza na askari na maofisa wa Jeshi hilo pamoja na kujua changamoto wanazokutananazo wakati wanapotekeleza majukumu yao ya kulinda usalama wa raia na mali zao.
Mkuu wa Jeshi la Polisi Nchini (IGP) Simon Sirro, akizungumza na baadhi ya askari wa Kikosi cha Usalama Barabarani katika mkoa wa Arusha, baada ya kukagua gwaride lililoandaliwa kwa ajili yake alipowasili katika mkoa huo kwa ziara ya kikazi ya siku mbili yenye lengo la kujitambulisha na kuzungumza na askari na maofisa wa Jeshi hilo pamoja na kujua changamoto wanazokutananazo wakati wanapotekeleza majukumu yao ya kulinda usalama wa raia na mali zao. Picha na Jeshi la Polisi.
Baadhi ya askari wa kikosi maalum cha kupambana na uhalifu wa kutumia silaha wakiwa tayari kwa kutoa heshima ya kijeshi kwa Mkuu wa Jeshi la Polisi Nchini (IGP) Simon Sirro, alipowasili katika mkoa wa Arusha, kwa ziara ya kikazi ya siku mbili yenye lengo la kujitambulisha na kuzungumza na askari na maofisa wa Jeshi hilo pamoja na kujua changamoto wanazokutananazo wakati wanapotekeleza majukumu yao ya kulinda usalama wa raia na mali zao. 


Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini (IGP) Simon Sirro (kulia), akizungumza na baadhi ya askari wa Jeshi hilo katika mkoa wa Arusha, wakati akiwa kwenye ziara ya kikazi ya siku mbili, ambapo aliwataka askari kufanyakazi kwa kufuata misingi ya sheria na taratibu za nchi wakati wanapotekeleza majukumu yao ya kazi za kipolisi. Picha na Jeshi la Polisi.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad