HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Tuesday, August 29, 2017

HAKUNA BASI KUONDOKA KATIKA KITUO CHA MABASI UBUNGO BILA KUFANYIWA UKAGUZI -SAMWIX

Mkuu wa Kituo cha Ukaguzi  wa Usalama barabarani wa Kituo cha Mabasi Ubungo, Ibrahim Samwix akizungumza leo baada ya kufanya ukaguzi amesema kuwa hakuna basi linaweza kuondoka katika kituo cha mabasi bila kufanyiwa ukaguzi.

Samwix amesema kuwa basi ambalo likibainika katika kituo cha Mabasi Ubungo lina makosa haliwezi kufanya safari zake ambapo amewataka wamiliki kufanya matengenezo ya mara mara ili kuondokana na adha ambazo watakuna nazo mara baada kufanya ukaguzi wa mabasi hayo.

Aidha amesema kuwa madereva wanatakiwa kuwa mabalozi wa kukataa kufanya safari zao pale wanapobaini kuwa basi lina ubovu wowote ili kupukana na ajali ambazo zinatokana na ubovu wa mabasi hayo.
Mkuu wa Kituo cha Ukaguzi  wa Usalama barabarani wa Kituo cha Mabasi Ubungo, Ibrahim Samwix akiwa ndani ya uvungu wa basi la Smart akifanya ukaguzi kabla ya basi hilo kuondoka leo jijini Dar es Salaam.
Mkuu wa Kituo cha Ukaguzi  wa Usalama barabarani wa Kituo cha Mabasi Ubungo, Ibrahim Samwix akifanya ukaguzi wa basi kabla halijaondoka kituo hicho leo jijini Dar es Salaam.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad