HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Thursday, July 20, 2017

SERA NA MIKATABA IKIANGALIWA ITAFUNGUA USHIRIKI WATANZANIA KATIKA SEKTA YA UWEKEZAJI -TNBC

Kaimu  Mkurugenzi Idara ya Ushiriki Watanzania katika sekta ya Uwekezaji wa  Baraza la  Taifa uwezeshaji wananchi Kiuchumu (TNBC) , Esther  Mmbaga akizungumza  katika ufunguzi wa mdahalo uliojikita  kuangalia uwekezaji  kwa kiasi gani watanzania  wanashiriki atika masuala ya uwekezaji kwenye mkutano uliofanyika  katika ukumbi wa Costech  leo jijini Dar es Salaam.
Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi  Isiyo ya Kiserikali inayojighulisha na Utafiti  wa Kisera  kwa ajili ya Kukuza Sayansi , Teknolojia  na Ubunifu (Stipro) Bitrina Diyamett  akizungumza juu utafiti wao waliofanya kupitia taasisi  hiyo katika kuangalia watanzania kunufaika katika masuala ya uwekezaji .
Mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Mzumbe , Profesa Honest Ngowi akizungumza juu masuala ya uwekezaji na utafiti uliofanywa na Taasisi ya Stipro leo jijini  Dar es Salaam.
Sehemu ya wadau katika wa mdahalo uliojikita  kuangalia uwekezaji  kwa kiasi gani watanzania  wanashiriki uliofanyika  katika ukumbi wa Costech  leo jijini Dar es Salaam.



Na Chalila Kibuda, Globu ya Jamii
Ushiriki watanzania katika  uwekezaji  wa katika  sekta ya madini na kilimo ni mdogo kutokana na mifumo  iliyopo na kufanya nchi kwa wazawa kushindwa kunufaika.

Akizungumza katika mdahalo  ulioandaliwa na Taasisi  Isiyo ya Kiserikali inayojighulisha na Utafiti  wa Kisera  kwa ajili ya Kukuza Sayansi , Teknolojia  na Ubunifu (Stipro), Kaimu  Mkurugenzi Idara ya Ushiriki Watanzania katika sekta ya Uwekezaji wa  Baraza la  Taifa uwezeshaji wananchi Kiuchumu (TNBC) , Esther  Mmbaga amesema kuwa baraza limeunda kitu cha kuweza kufatilia mikataba na sera  namna ya wazawa  wanavyoshiriki katika uwekezaji.

Amesema  ushiriki watanzania katika uwekezaji kuanzia ajira na hata bidhaa zinazozalishwa nchini  hazitumiki kwa wawekezaji kutokana na madai kuwa hazina ubora.

Mmbaga amesema kutokana na ukosekanaji wa ushiriki Baraza litaweka utaratibu kwa kila kinachofanyika  nchini chi ya uwekezaji watanzania waweze kushiriki au kufanya ubia kwa teknolojia kuandaa utaalam wa uzalishaji wa taaluma.

Amesema kuwa tafiti hizo ndizo zinafanya baraza kufanyia  kazi katika kuangalia wazawa wanavyonufaika na  uwekezaji unaofanywa nchini.

Nae  Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi  Isiyo ya Kiserikali inayojighulisha na Utafiti  wa Kisera  kwa ajili ya Kukuza Sayansi , Teknolojia  na Ubunifu (Stipro) Bitrina Diyamett  amesekuwa utafiti  huo ulijikita  kuangalia uwekezaji  kwa kiasi gani watanzania wanashiriki.

Amesema watu wanafanya uwekezaji  nchini  lakini hawanunui bidhaa za ndani  na kuonekana  watanzania sio  sehemu ya uwekezaji hali ambayo inahitaji kuangalia sera  pamoja na mikataba.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad