Wananchi mbalimbali wakipata huduma kwenye banda la NHIF ambapo kampeni ya usajili wa
Toto Afya Kadi unafanyika.
Na Mwandishi Wetu
KAMPENI ya usajili wa watoto chini ya Umri wa miaka 18 unaofanywa na Mfuko
wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF) kwenye maonesho ya 41 ya Sabasaba, umekuwa
kivutio kikubwa ambapo wazazi na walezi wamepongeza mpango huo.
NHIF inaendesha kampeni hiyo chini ya mpango wa Toto Afya Kadi ambapo
wazazi na walezi wanawasajili watoto wao kwa gharama ya shilingi 50,400 na
kupatiwa kitambulisho cha matibabu kitakachomwezesha kupata huduma hizo
ndani ya nchi.
Kaimu Mkurugenzi wa Huduma za Tiba na Ushauri wa Kiufundi Dr. Aifena Mramba akitoa
maelezo kwa wananchi waliofika bandani hapo.
Wakizungumza kwa nyakati tofauti bandani hapo, Mkazi wa Kinondoni Bw. Ally
Raymond amepongeza Mfuko kwa kuja na mpango huo ambao umekuwa ni wa
nafuaa kwa wazazi na walezi ambao hawakuwa na fursa ya kupata huduma hizo.
“Kwa kweli hii ni hatua kubwa lazima tuwapongeze hasa kwa kuwajali watoto
hawa chini ya umri wa miaka 18 ambao hasa ndio wana uhitaji mkubwa wa
matibabu hivyo name nitoe wito kwa wazazi wengine kutumia fursa hii ili kuwa na
uhakika wa matibabu wa watoto wao,” alisema Bw. Raymond.
Mzazi mwingine alipongeza hatua ya NHIF ya kusajili na kutoa vitambulisho hivyo
baada ya siku moja hatua ambayo imeondoa usumbufu kwa wanaohitaji kusajili
watoto wao.
Usajili wa Toto Afya Kadi ukiendelea.
Akizungumza bandani hapo Kaimu Mkurugenzi wa Masoko na Utafiti, Bi. Angela
Mziray alisema kuwa hii ni fursa nzuri kwa wazazi na walezi ya kupata
vitambulisho vya matibabu na kuwa na uhakika wa kupata matibabu wakati
wowote na kuondokana na usumbufu ambao wangeweza kuupata.
Alisema kuwa NHIF imeanzisha mpango huo kutokana na umuhimu wa kundi la
watoto ambao wameonekana kuwa na uhitaji mkubwa wa kulindwa kwa
kuhakikishiwa huduma za matibabu. Jumla ya watoto 150 wameshasajiliwa na
kupatiwa vitambulisho vyao.
Mbali na huduma ya usajili wa watoto, Mfuko pia unatoa huduma ya elimu kwa
juu ya huduma za Bima ya Afya lakini pia kushughulikia kero mbalimbali za
wanachama.
Wananchi wakilipia gharama za usajili wa Toto Afya Kadi kwa Maofisa wa Benki ya NMB.
Kaimu Mkurugenzi wa Masoko na Utafiti Anjela Mziray akitoa maelezo ya huduma juu ya
mpango wa Toto Afya Kadi.
Ofisa Masoko na Elimu kwa Umma Grace Michael akikagua fomu za watoto ambazo zimejazwa
kwa ajili ya vitambulisho vya matibabu.
Elimu kwa umma na uchukuaji wa fomu za watoto ukiendelea.
Maofisa wa NHIF wakitoa huduma kwa wananchi.
No comments:
Post a Comment