HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Thursday, June 15, 2017

MADAKTARI WA KICHINA WAJITAMBULISHA NA KUAGA

 Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein (kulia) alipokuwa akizungumza na Ujumbe wa Madaktari wa Kichina wanaotoa huduma katika Hospitali mbali mbali za Unguja na Pemba wakiongozwa na Balozi Mdogo wa China anayefanyia kazi Zanzibar Mhe.Xie Xiaowu (wa tatu kulia) katika mazungumzo yao aliwakaribisha Madakatari 21 wapya na kuwaaga 21 waliomaliza muda kutoka  Jamhuri ya Watu wa China katika ukumbi wa Ikulu Mjini Unguja leo.
 Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein (kulia) alipokuwa akizungumza na Ujumbe wa Madaktari wa Kichina unaoongozwa na Balozi Mdogo wa China anayefanyia kazi Zanzibar Mhe.Xie Xiaowu (wa pili kushoto) katika mazungumzo yao Rais aliwakaribisha Madakatari 21 wapya na kuwaaga 21 waliomaliza muda kutoka  Jamhuri ya Watu wa China (hawapo pichani) katika ukumbi wa Ikulu Mjini Unguja leo,(kushoto) Kiongozi wa Madakatari waliomaliza muda Xu Zhuoqun.
 Baadhi ya Madakatari wa Kichina waliofika Ikulu Mjini Unguja kuoanana na Rais leo ambapo jumla yao ni  Aroubaini na mbili wakiwemo wapya Ishirini na moja wanaomaliza muda wao wa kazi waliofika kumuaga Rais na Ishirini na Moja walikaribishwa na Rais katika mazungumzo yaliyofanyika Ikulu Mjini Unguja.
 Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein (katikati) akiwa katika picha ya pamoja na  Ujumbe wa Madaktari wa Kichina unaoongozwa na Balozi Mdogo wa China anayefanyia kazi Zanzibar Mhe.Xie Xiaowu (wa nne kushoto) baada ya mazungumzo na kuwaaga Madaktari hao waliomaliza muda wao wa kazi hapa Nchini, leo walipofika Ikulu Mjini Unguja.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein (kulia) akimkaribisha Kiongozi wa Madaktari wapya Ishirini na moja kutoka Jamhuri ya Watu wa China Wang QI baada ya mazunguzo na Madaktari hao waliofika Ikulu Mjini Unguja leo wakiongozwa na Balozi Mdogo wa China anayefanyia kazi Zanzibar Mhe.Xie Xiaowu (katikati) Kiongozi wa Madaktari waliomaliza muda Xu Zhuoqun.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad