Askari
Polisi nchini Uingereza, wakimtia mbaroni mtuhumiwa mmoja
aliyetambulika kwa Jina la Omega Mwaikambo aliyedaiwa kupiga picha ya
mwili wa mtu aliyefariki uliokuwemo kwenye mfuko maalum wa kuhifadia
maiti inayodhaniwa kuwa ilitokana na ajali ya moto katika jengo la
Grenfell Tower iliyotokea hivi karibuni jijini London huko nchini
Uingereza kisha kuziweka kwenye mitandao ya kijamii.
Inadaiwa
kuwa mtuhumiwa huyo, alifanya hivyo siku ya jumatano asubuhi, alipotoka
nje ya nyumba yake na kukuta mfuko huo wenye mwili na kuufungua kisha
kuupiga picha na kurekodi video alizoziweka kwenye mtandao wa Facebook
huku akiuliza "Je, kuna mtu yeyote anaujua mwili huu ambao uko nje ya
ghorofa langu kwa zaidi ya saa mbili?"
Mtuhumiwa
huyo ambaye anaishi eneo la jirani kabisa na jengo la Grenfell Tower
lililopatwa na janga la kuteketea kwa moto alipandishwa kizimbani jana
Juni 16, 2017 katika Mahakama ya Hakimu Westminster na kusomewa mashtaka
yake na kuhukumiwa kwenda jela kwa miazi mitatu kwa kutenda kosa hilo.
No comments:
Post a Comment