HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Tuesday, May 2, 2017

PPF WAUNGANA NA WENZAO KUADHIMISHA SIKU YA WAFANYAKAZI DUNIANI

NA K-VSI BLOG/Khalfan Said
WAFANYAKAZI wa Mfuko wa Pensheni wa PPF, wameungana na wenzao jijini Dar es salaam kuadhimisha siku ya wafanyakazi Duniani maarufu kama Mei Mosi.

Kitaifa sherehe hizo zinaongozwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. John Pombe Magufuli mjini Moshi ambapo kauli mbiu ya mwaka huu ni “Uchumi wa Viwanda uzingatie Haki, Maslahi na Heshima ya wafanyakazi.”

Aidha jijini Dar es Salaam, Wafanyakazi wa PPF na wengine kutoka sekta ya Umma na Binafsi, walifanya matembezi kutoka eneo la Mnazi Mmoja hadi uwanja wa Uhuru huku wakiongiozwa na brass band ya Jeshi la Magereza.

Kwa upande wao wafanyakazi wa PPF  walianza kwa kukusanyika kwenye ofisi za Makao Makuu ya Mfuko huo barabara ya Samora/Morogoro ambapo walipewa maelekezo ya umuhimu wa ushiriki wao katika maetembezi hayo na kujiunga na wenzao eneo la kuanzia matembezi pale Mnazi moja.
Mgeni rasmi katika sherehe za Mei Mosi jijini Dar es Salaam, alikuwa Mkuu wa Wilaya ya Temeka, Bw. Felix Lyaviva, ambaye alipokea maandamano ya wafanyakazi na magari kadhaa kutoka taasisi za umma na binafsi yakionyesha huduma zitolewazo na taasisi hizo.
Huduma zitolewazo na PPF ni pamoja na kulipa Mafao ya Uzeeni, Mafao ya Wategemezi,Mafao ya Elimu, Mafao ya Kiinya Mgongo, Mafao ya Kifo, Mafao ya Ugonjwa na Mafao ya Uzazi. Lakini pia kazi nyingine za Mfuko huo ni kusajili wanachama kupitia mfumo wa uchangiaji wa hiari ujulikanao kama “Wote Scheme”.
Baadhi ya wafanyakazi wa PPF, wakiwa kwenye matembezi ya kuadhimisha Mei Mosi jijini Dar es Salaam Leo.


Kiongozi wa kundi la wafanyakazi WA PPF, wwlioshiriki matembezi ya kuadhimisha siku ya wafanyakazi duniani, Mohammed Siaga, (kushoto), akizungumza muda mfupi kabla ya kuanza matembezi hayo.















No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad