HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Tuesday, May 9, 2017

NSSF YATOA SEMINA KWA KIKUNDI CHA UMOJA WA MIRADI YA VIZIWI TANZANIA

SHIRIKA la Taifa la Hifadhi ya Jamii (NSSF) limetoa semina juu ya umuhimu wa hifadhi ya jamii kwa wanacama wa kikundi cha Umoja wa Miradi ya Viziwi Tanzania UMIVITA.

Semina hiyo ilitolewa mwishoni mwa wiki na shirika hilo ambapo ilihusisha wanachama wapatao mia mbili.

Akizungumza katika semina hiyo Ofisa Matekelezo Mkuu wa NSSF Mkoa wa Temeke, Nuhu Ramadhani alisema wanachama hao walipata fursa ya kuifahamuvizuri NSSF na kujua mafao yanayotolewa na shirika hilo yakiwemo pensheni ya uzeeni,pensheni ya ulemavu,pensheni ya urithi, msaada wa mazishi, mafao ya kuumia kazini, mafao ya uzazi na matibabu bure kwa mwananchama na wategemezi wake.

Aisha NSSF ilitoa fursa kwa Wanachama wa UMIVITA waliohudhuria semia hiyo kujiandikisha kuwa wanachama.
Ofisa Uhusiano na Masoko wa NSSF, Anna Nguzo, akizungumza wakati wa semina iliyoandaliwa na NSSF wa ajili ya wanachama wa Kikundi cha Umoja wa Miradi kwa Viziwi Tanzania.

Ofisa Matekelezo Mwandamizi wa NSSF Mkoa wa Temeke, Naphisa Jahazi, akizungumza wakati wa semina hiyo.

Mwenyekiti wa Umoja wa Miradi kwa Viziwi (UMIVITA), Jamal Amiri akizungumza wakati wa semina iliyoandaliwa na NSSF kwa ajili ya wanachama wa Kikundi cha Umoja wa Miradi kwa Viziwi Tanzania.

Wanasemina.
Baadhi ya wanasemina.

Baadhi ya maofisa wa NSSF wakiwa katika semina hiyo.

Ofisa Matekelezo Mkuu wa NSSF Mkoa wa Temeke, Nuhu Ramadhani akitoa mada kuhusu Mafao yatolewayo na NSSF wakati wa semina iliyoandaliwa na NSSF wa ajili ya wanachama wa Kikundi cha Umoja wa Miradi kwa Viziwi Tanzania (UMIVITA).

Ofisa Matekelezo Mkuu wa NSSF Mkoa wa Temeke, Nuhu Ramadhani akitoa mada kuhusu Mafao yatolewayo na NSSF wakati wa semina iliyoandaliwa na NSSF wa ajili ya wanachama wa Kikundi cha Umoja wa Miradi kwa Viziwi Tanzania (UMIVITA).

Wanasemina wakipewa vipeperushi vyenye taarifa kuhusu Mafao yatolewayo na NSSF.

Tunajifunza kuhusu mafao ya NSSF.

Wanasemina wakipewa vipeperushi vyenye taarifa kuhusu Mafao yatolewayo na NSSF.

Baadhi ya wanachama wa Kikundi cha Umoja wa Miradi kwa Viziwi Tanzania (UMIVITA) wakiwa katika semina hiyo.

Baadhi ya wanachama wa kikundi cha Umoja wa Miradi kwa Viziwi Tanzania (UMIVITA) wakiwa katika semina kuhusu ya Mafao yatolewayo na Mfuko wa NSSF.

Mwenyekiti wa Umoja wa Miradi kwa Viziwi (UMIVITA), Jamal Amiri akizungumza na waandishi wa habari wakati wa semina iliyoandaliwa na NSSF wa ajili ya wanachama wa Kikundi cha Umoja wa Miradi kwa Viziwi Tanzania kuhusu mafao yatolewayo na NSSF. Kulia ni mkalimali wake.

Ofisa Matekelezo Mwandamizi wa NSSF Mkoa wa Temeke, Siaeli Moshi akijibu maswali yaliyoulizwa na washiriki wa semina hiyo. Kushoto kwake ni mkalimani wa washiriki wa semina hiyo.
Ofisa Matekelezo wa NSSF Mkoa wa Temeke, Masanyika Choka, akijaza fomu za kujiunga na NSSF baadhi ya wanachama wa Kikundi cha Umoja wa Miradi kwa Viziwi Tanzania (UMIVITA).

Ofisa Matekelezo wa NSSF Mkoa wa Temeke, Masanyika Choka, akitoa maelekezo kwa baadhi ya watu wenye ulemavu wa kusikia (viziwi), wakati wa semina iliyotolewa na NSSF kwa wanachama wa Kikundi cha Umoja wa Miradi kwa Viziwi Tanzania (UMIVITA).

Ofisa Matekelezo Mwandamizi wa NSSF Mkoa wa Temeke, Naphisa Jahazi akijaza fomu ya kujiunga na NSSF mmoja wa wanachama wa kikundi cha UMIVITA.

Ofisa wa NSSF akiwaandikisha baadhi ya wanachama wa UMIVITA kujiunga na NSSF.

Ofisa Matekelezo wa NSSF Mkoa wa Temeke, Masanyika Choka, akiwaandikisha baadhi ya watu wenye ulemavu wa kusikia (viziwi), wakati wa semina iliyotolewa na NSSF kwa wanachama wa Kikundi cha Umoja wa Miradi kwa Viziwi Tanzania (UMIVITA).

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad