SHINDANO la Urembo la kumsaka mnyange wa Chuo cha Ustawi wa Jamii kwa mwaka 2017/18, linatarajiwa kufanyika siku ya ijumaa, Mei 19 katika Ukumbi wa King Solomon, Namanga jijini Dar es Salaam.
Akizungumza na Mtaa kwa Mtaa jijini Dar es Salaam, Mwalimu wa Warembo hao, Clara Nyaki amesema maandalizi yanaendelea kufanyika kwa ustadi mkubwa huku kila mrembo akiwa ni mwenye hari ya kutaka kunyakua taji hilo, hivyo mshindi atakayepatikana atakuwa ameonyesha uwezo wake binafsi ikilinganishwa na wengine wataofuata.
Akizungumza na Mtaa kwa Mtaa jijini Dar es Salaam, Mwalimu wa Warembo hao, Clara Nyaki amesema maandalizi yanaendelea kufanyika kwa ustadi mkubwa huku kila mrembo akiwa ni mwenye hari ya kutaka kunyakua taji hilo, hivyo mshindi atakayepatikana atakuwa ameonyesha uwezo wake binafsi ikilinganishwa na wengine wataofuata.
Clara amesema siku hiyo itakuwa ya kipekee kutokana na namna walivyojipanga hasa kutokana na urembo walionao warembo wenyewe. Pia, amewakaribisha Watanzania wote kwa ujumla kufika siku hiyo ili kushuduhia tukio hilo.
Kwa upande wao Walimbwende hao wamesema wamejiandaa kila mmoja kuondoka na ushindi kulingana na maandalizi waliyoyafanya katika kipindi chote walichokuwa na mwalimu wao.
Warembo watakaojimwaga siku hiyo ni Ruth Deouratius ,Melody Thomas, Elizabeth Julius, Careen Kileo, Loyce Jeck ,Diana Wambura , Angela Milanzi pamoja na Elice Mwakajila .
Kwa upande wao Walimbwende hao wamesema wamejiandaa kila mmoja kuondoka na ushindi kulingana na maandalizi waliyoyafanya katika kipindi chote walichokuwa na mwalimu wao.
Warembo watakaojimwaga siku hiyo ni Ruth Deouratius ,Melody Thomas, Elizabeth Julius, Careen Kileo, Loyce Jeck ,Diana Wambura , Angela Milanzi pamoja na Elice Mwakajila .
Warembo wakiwa katika picha ya pamoja kwa pozi mbalimbali watavyokwenda
katika kinyanganyilo hicho kitachofanyika Mei 19 katika ukumbi wa King
Solomon jijini Dar es Salaam.
No comments:
Post a Comment