HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Wednesday, May 3, 2017

Meya wa jiji amtembelea Mjane wa Bob Makani nyumbani leo

Inline image 1
Meya wa jiji la Dar es Salaam, Isaya Mwita akimfariji Mjane wa aliyekuwa mhasisi na Katibu Mkuu wa kwanza wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) Bob Makani (Mama Makani)
Inline image 2
Mjane wa aliyekuwa mhasisi na Katibu Mkuu wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) Kaboga Makani akimueleza jambo Mstahiki Meya wa jiji la Dar es Salaam Isaya Mwita mara baada ya kumtembelea Nyumbani kwake mapema leo asubuhi.
Inline image 3
Meya wa jiji la Dar es Salaam, Isaya Mwita akiwa kwenye picha ya pamoja na familia ya Mahasisi na Katibu Mkuu wa kwanza wa Chadema Bob Makani, wa kwanza kulia ni mtoto wa mzee Makani , Mohamed Mkani, na katikati ni mke wa Bob Makani Kaboga Makani.
Inline image 4
Inline image 1
Inline image 2


Meya wa jiji la Dar es Salaam akiwa na familia ya Mjane wa aliyekuwa muwasisi na Katibu mkuu wa kwanza wa Chadema.
Inline image 3
Inline image 4

Picha zote na Christina  Mwagala, OMJ.



NA CHRISTINA MWAGALA, OMJ
MEYA wa jiji la Dar es Salaam Isaya Mwita leo amemtembele mjane wa aliyekuwa Mhasisi na Katibu Mkuu wa kwanza wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) Bob Makani , Mama Kaboga Makani ikiwa ni moja ya ziara zake za kutembelea wazee pamoja na viongozi ambao waliwahi kushika nafasi mbalimbali za uongozi ndani ya jiji la Dar es Salaam.

Meya ambaye amerejea Nchini jana kutoka Nchini Iran ambapo alikuwa kwa ziara ya kikazi ya siku 10, amesema kwamba hatua ya kutembelea viongozi pamoja na wazee ambao ni waasisi inalenga kutambua michango yao katika nafasi ambazo waliwahi kutumikia na kwamba busara zao pia ndio zimeweza kulifikia Taifa sehemu ilipo hivi sasa.

Alifafanua kuwa Bob Makani enzi za uhai wake alikuwa ni mmoja na mwasisi wa Chadema na kwamba anatambua mchango wake kutokana na juhudi alizozionyesha ikiwemo kukipigania chama hadi kufikia kilipo hivi sasa.

Alisema Bob Makani pamoja na wenzake ndio waliokianzisha Chama Cha Chadema na kufika mbali zaidi kwamba bila wao hata yeye asingekuwa Meya wajiji hili kupitia chama hicho na kwamba mchango wao ndani ya chama bado utaendelea kukumbukwa na kila mmoja wakiwemo wanachama wa chama hicho na wananchi kwa ujumla.

Alisema Bob Makani mbali na kuwa mwanachama na mwasisi wa Chadema lakini pia aliwahi kuwa Gavana wa Benki kuu ambapo alitumikia nafasi hiyo kwa na hivyo baada ya kustaafu nafasi hiyo aliamua kuanzisha chama na hivyo kuwepo hadi hivi sasa.

“ Haya sio mambo ya kisaisa , lakini unaweza kuona kwamba ni alikuwa mtu muhimu , lakini pia kama kijana wao lazima nipate basara kutoka kwao, ingawaje hatunaye tena hapa duniani, lakini huko alipo anaona jambo gani ambalo tunafanya kama vijana ambao alituacha ndani ya chama” alisema.

Alifafanua kwamba jambo la kutembelea viongozi ama waasisi wa nafasi chama sio jambo la kisiasa bali ni kutokana na kutambua mchango wakazi ambazo waliwahi kuzifanya wakati huo.

“ Ziara hii sio ya kwa Mzee Makani tu, ila ni kwa waasisi , na wale ambao waliwahi kuwa viongozi wa jiji, wapo nitawatembelea, ikiwa ni sehemu yangu pia ya kutambua mchango wao, sambamba na kupata baraka , busara zao ambazo walizitumia katika uongozi wao, ukizungumza vizuri na wazee hawa unapata baraka na kuona kwamba namna gani unaweza kuwaongoza wananchi” alisema Meya Mwita.

“ Nimekuja leo kumuona Mama yetu, naweza kusema ni mama yetu kwa sababu kila mmoja anamfahamu mzee Makani , alikipigania chama, na ndio katibu mkuu wa wa kwanza ndani ya Chadema, kama vijana hatuna sababu ya kuwasahau wasisi wetu, wazee wetu, watu ambao tunawatambua kabisa waliitumikia nchi yetu” alisema Meya Isaya.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad