HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Thursday, May 25, 2017

MBUNGE WA ILEMELA AIKARIBISHA TIMU YA MBAO FC BUNGENI

Mbunge wa jimbo la Ilemela na Naibu Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Dkt Angeline Mabula hii leo ameikaribisha bungeni timu ya mpira wa miguu ya Ilemela Jijini Mwanza Mbao Fc 

Ikumbukwe kuwa huu ni mwendelezo wa jitihada za mbunge huyo za kuhakikisha anainua michezo katika jimbo la Ilemela na kutoa fursa kwa vijana kuonyesha na kuvitumia vipaji walivyonavyo katika kujiongezea kipato, Mhe Dkt Angeline Mabula amesema 

‘… Huu ni mwendelezo wa jitihada za kila siku ninazozifanya za kuhakikisha tunaboresha michezo yetu lakini pia kuifanya kuwa chanzo cha kipato katika kuendesha maisha ya kila siku ya vijana wetu wa Ilemela na Tanzania kwa ujumla wake …’

Nao wachezaji wa Timu hiyo wamemshukuru Mbunge wao Dkt Angeline Mabula  kwa jitihada zake za kuboresha na kukuza michezo jimboni humo huku wakimuahidi ushindi katika mechi yao ya hatua ya fainali ya Kombe la FA dhidi ya Timu ya Simba ya Jijini Dar es Salaam wanayotarajia kuicheza siku ya jumamosi mjini Dodoma 

“ Ilemela ni yetu, tushirikiane kuijenga ”

Imetolewa na
Ofisi ya Mbunge 
Jimbo la Ilemela
25.05.2017

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad