HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Monday, May 8, 2017

BALOZI ASHA-ROSE MIGIRO AWATEMBELEA WANADIASPORA READING

Balozi wa Tanzania nchini Uingereza, Mhe. Asha-Rose Migiro alifanya ziara ya kuwatembelea watanzania waishio Reading na Bekshire tarehe 6/5/2017. Wakati wa ziara hiyo Mhe. Balozi Migiro alipata fursa ya kufanya mkutano na kuwatembelea baadhi ya watanzania hao kwenye maeneo yao ya kazi.
Balozi wa Tanzania nchini Uingereza, Mhe. Asha-Rose Migiro akiwa pamoja na baadhi ya wana diaspora waishio Reading na Bekshire waliohudhuria mkutano.
 Balozi wa Tanzania nchini Uingereza Mhe. Asha-Rose Migiro akisalimiana na Bw. Daniel Samwenda mmoja wa wamiliki wa kampuni ya McDaan Finance inayojishughulisha na shughuli mbali mbali za kifedha kama kutoa mikopo ya muda mfupi.
 Balozi wa Tanzania nchini Uingereza, Mhe. Asha-Rose Migiro akipata maelezo kutoka kwa Bw. Hassan Abdula Mkurugenzi wa Kampuni ya Hill View Family Co. Ltd inayojishughulisha na usafirishaji wa mizigo.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad