HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Wednesday, April 19, 2017

VIDEO: HIVI NDIVYO DALADALA LILILOPIGA MWELEKA NA KUINGIA MTARANO LINAVYOONEKANA

Basi la abiria linalofanya safari zake kati ya Makumbusho mpaka Posta, limepiga mweleka na kuingia mtaroni katika eneo la Oysterbay, Kinondoni jijini Dar es salaam mchana wa leo.

imeelezwa kwamba Basi hilo lenye namba za usajili T 958 DEJ aina ya Hino lililokuwa likitokea Posta kuelekea upande wa Moroco, lilijikuta likiingia mtaroni humo, baada ya dereva wake kushindwa mbinu za kulizuia kufuatia gari nyingine iliyoingia ghafla barabarani ikitokea upande wa Kituo cha Polisi Oysterbay, hivyo kutokana mwendo kasi wa basi hilo, ilishindwa kusimama na kuparamia mti uliokuwa kando ya barabara na kuingia mtaroni.

Inadaiwa kuwa abiria wote waliokuwepo kwenye basi hilo walitoka salama na kuendelea na safari zao.
Hivi ndivyo muonekano wa Basi hilo baada ya kuparamia mti.
Mashuhuda wa Ajali hiyo wakiwa katika eneo la tukio.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad