HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Thursday, April 13, 2017

MWILI WA DK MACHA KUWASILI APRILI 20

Mwili wa Mbunge wa Viti Maalumu (Chadema), Dk Elly Macha unatarajiwa kuwasili nchini Aprili 20 mwaka huu ukitokea nchini Uingereza.
Dk Macha alifariki dunia Machi 31 mwaka huu katika Hospitali ya New Cross, Wolverhampton nchini Uingereza alikokuwa akitibiwa.
Akitoa ratiba ya msiba huo leo bungeni, Spika wa Bunge, Job Ndugai alisema taratibu zote za Uingereza za kurudisha mwili wa Mbunge huo zimekamilika.
“Kule kuna taratibu nyingi za kisheria na kadhalika haikuwa rahisi kuharakisha mchakato huo, tunashukuru ubalozi wetu wa nchini humo umeweza kufanikisha jambo hili,”amesema
Ndugai amesema mwili wake utawasili alhamis ya wiki ijayo katika uwanja wa Ndege wa kimataifa wa Mwalimu Julius Nyerere April 20, mwaka huu saa tisa.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad