HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Wednesday, April 12, 2017

MSICHANA ANAYEUGUA UGONJWA WA KUZEEKA AFARIKI A. KUSINI

Afrika Kusini inaomboleza kifo cha Ontlametse Phalatse, msichana wa umri wa miaka 18 ambaye alikuwa anaishi na ugojwa unaojulikana kama Progeria, ambayo ni hali ya kimaumbile isiyo ya kawaida ambayo husababisha mtu kuzeeka kwa haraka.
Mwezi uliopita Ontlametse alisherehekea siku ya kuzaliwa na rais wa Afrika Kusini Jacob Zuma.
Seriklia ya Afrika kuisni imeongoza taifa kutuma rambi rambi kufuatia kifo hicho.
Alifariki hiyo jana katika hospitali ya Dr George Mukhari Academic iliyo nje ya mji wa Pretora.
Phalatse alikuwa mmoja wa wasichana wawili waliokuwa na hali hiyo nchini Afrika Kusini.
Alijiita "mama wa kwanza" , baada ya kuwa mtoto wa kwanza mweusi nchini Afrika Kusini, kupatikana akiwa na ugonjwa wa Progeria.
Alitajwa kuwa mtoto wa kuwapa watu motisha na mtot wa miujiza baada ya kuishi kuliko matarajio walioyokuwa nayo madaktari waliosema kuwa angefariki miaka minne iliyopita.
Rais Zuma ametuma rambi rambi zake kwa familia ya msichana huyo.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad