HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Tuesday, April 18, 2017

MAKAMU WA RAIS MHE. SAMIA AKUTANA NA VIONGOZI WA UWT ZANZIBAR

Mjumbe wa Kamati Kuu ya CCM na Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akizungumza na Viongozi wa UWT kutoka mikoa minne ya Unguja.
Mjumbe wa Kamati Kuu ya CCM na Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akizungumza na Viongozi wa UWT Unguja ambapo aliwaambia washikamane katika kukitetea Chama kilichobeba maana halisi ya Mapinduzi na alihimiza Vijana wapewe nafasi kwa wingi kwani wao wananguvu na kasi ya siasa ya wakati huu.
Waziri wa Kazi,Uwezeshaji,Wazee,Vijana,Wanawake,na Watoto Mhe, Maudline Castico akizungumza wakati wa mkutano wa Mjumbe wa Kamati Kuu CCM na Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan na Viongozi wa UWT Unguja .
Mke wa Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Mama Asha Suleiman Iddi akizungumza kwenye mkutano wa Mjumbe wa Kamati Kuu ya CCM ambaye pia ni Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan na Viongozi wa UWT kwenye ukumbi wa NEC Afisi Kuu Kisiwandui, Zanzibar.
Mjumbe wa Kamati Kuu ya CCM na Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akisalimiana na wasanii wa Filamu nchini maarufu kama Bongo Movie waliopita kumsabahi kwenye Makao Makuu ya CCM, Kisiwandui Zanzibar.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad