Na Zainab Nyammka, Globu ya Jamii
Msafara wa mabingwa wa watetezi wa ligi kuu Tanzania bara Yanga SC , umewasili salama jijini Dar es salaam ukitokea Morogoro walipokwenda kucheza na Mtibwa Sugar kwa matokeo ya sare ya 0- 0.
Msafara huo umeelekea moja kwa moja kambini kwa maandalizi ya michezo miwili muhimu itakayofanyika kesho machi 7, 2017 dhidi ya Kiluvya United uwanja wa Taifa na machi 11, klabu bingwa Afrika dhidi ya Zanaco FC.
Timu imeendelea na mazoezi jioni ya leo kwa ajili ya kujiandaa na mchezo wa kesho robo fainali kombe la FA dhidi Kiluvya ya kutoka mkoani Pwani .
Kocha mkuu wa Yanga George Lwandamiana amesema kuwa licha ya ratiba ngumu kuikabili timu yake lakini amesema yupo tayari kupambana na vijana wake ili kuhakikisha klabu inapata matokeo mazuri katika michezo yote miwili.
Wapenzi , wanachama , mashabiki na wadau wa soka mnaombwa kujitokeza kwa wingi katika michezo yote miwili ili kuipa sapoti timu hiyo .
No comments:
Post a Comment