HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Wednesday, March 22, 2017

UONGOZI WA AZAM WALAANI VIKALI VURUGU WALIZOFANYIWA, YAKUBALI MATOKEO YA KUFUNGWA

 Ofisa habari wa Azama Jaffar Iddy 

Na Zainab Nyamka, Globu ya Jamii.
Klabu ya soka ya Azam fc, iliyokuwa  imelaani vikali  vitendo vya vurugu zilifanywa na timu ya Mbabane swallows katika mchezo ulifanyika nchini Swazland mchezo ambao walikubali kipigo cha goli 3-0, na kusema wao wanaliachilia mbali suala hilo wakijua CAF ndio wenye maamuzi ya mwisho.

 Azam ilikuwa ikishiriki kwenye ikishiriki michuano ya Kombe la Shirikisho Barani Afrika CAF iliondolewa kwenye michuano hiyo baada ya kushindwa kulinda ushindi wao wa nyumbani wa goli 1-0  na kutolewa kwa jumla ya goli 3-1 mwishoni mwa wiki hii.

Akizungumzia tuhuma zilizokuwa juu yao kuwa waliwafanyia fujo Mbabane kwenye mechi ya awali iliyochezwa  jijini Dar es saalm, katika uwanja wa Chamazi complex, Ofisa habari wa Azama Jaffar Iddy amesema kuwa hizo taarifa hazina ukweli.

Iddy amesema sababu ambazo zimesambaa kuwa waliwafanyia fujo Mbabane  sio za kweli bali waliamua tu kutengeneza sababu kwao kuhakikisha wanatimiza azma yao,ambayo  anaamini ndiyo iliyopelekea klabu hiyo kupata matokeo hasi.

Amesema kwa matokeo waliyoyapata ya kufungwa mabao 3-0, kimpira wameyakubali lakini walicheza katika mazingra magumu sana kwa kuwa waliwachezesha wachezaji ambao walikuwa na majeraha kama Salum abubakari( sure boy) ,akisumbuliwa na dole gumba, Himid mao bega na Frank Domayo akisumbuliwa na Malaria..

Amesema katika mchezo wa mpira, yote huwa yanatokea katika uhalisia wa matokeo ya mpira ambayo yapo matatu, kufungwa, kushindwa na kutoka sare, hivyo basi wamekubali wamashindwa lakini wao kama Azam fc, jukumu la nini? Kifanyike! baada ya wao kufanyiwa vurugu zile ni jukumu la mechi kamishna maana ndiye alikuwa msimazi wa mchezo hule.

Pia amesema ingawa wameingia kambini na wachezaji wachache waliopo huku nane(8) wakiitwa kikosi cha timu ya Taifa, (Taifa stars), tayari kwa mchezo wao  na Yanga, unaotarajia kufanyika April mosi mwaka huu, na FA CUP, wanasumbuliwa na baadhi ya wachezaji ambao anaamini wanaweza kukosa michezo kaza inayowakabili, kama Kingu na John bocco, ambaye walimuacha Afrika kusini kwa matibabu Zaidi.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad