HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Friday, March 17, 2017

RAIS WA TFF AREJEA, AZUNGUMZIA UCHAGUZI WA CAF

Na Zainab Nyamka, Globu ya Jamii

JOPO la viongozi wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Nchini (TFF) limeingia mchana huu kutoka Addis Ababa, Ethiopia kulipokuwa na uchaguzi mkuu wa Shirikisho la Mpira barani Afrika (CAF) uliofanyika jana.

Katika uchaguzi huo mgombea Ahmad Ahmad kutoka nchini Madagascar alimuangusha aliyekuwa rais wa Shirikisho hilko Issa Hayotou kwa kipindi cha miaka 29 kwa kura 34 kwa 20.

Rais wa TFF, amesema kuwa uchaguzi ulikuwa ni wa haki na umeonyesha mabadiliko makubwa sana katika maendeleo ya soka barani Afrika na amewaahidi wwatashirikiana nae bega kwa bega.

Kabla ya kwenda Addis Ababa, Malinzi hakuweka wazi kuwa kura yake atampa nani kwani aliamini wote ni wazuri na wanafanya kazi zao kwa uweledi mkubwa,

Viongozi wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Nchini (TFF) wakiongozwa na Rais Jamali Malinzi (wa kwanza kulia) wakiwa katika picha ya pamoja baada ya kuwasili Nchini kutokea Addis Ababa, Ethiopia kwenye uchaguzi wa Shirikisho la Mpira wa Miguu barani Afrika (CAF).
 Rais wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Nchini (TFF) akizungumza na waandishi wa habari mara baada ya kuwsili uwanja wa ndege kutoka Addis Ababa Ethiopia kulipokuwa na uchaguzi Shirikisho la Mpira wa Miguu barani Afrika (CAF).
  Mwenyekiti wa zamani wa Chama cha soka cha Mpira (FAT) na mjumbe wa heshima wa  Shirikisho la Mpira wa Miguu barani Afrika (CAF) Said El maamury  akizungumza na waandishi wa habari mara baada ya kuwsili uwanja wa ndege kutoka Addis Ababa Ethiopia kulipokuwa na uchaguzi Shirikisho hilo.




No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad