
Waziri Mkuu wa Ethiopia ,Hailemariam Dessalegn akishuka kwenye ndege mara baada ya kuwasili katika uwanja wa Kimataifa wa Julius Nyerere mapema leo mchana,na baadae kupokelewa na mwenyeji wake Rais Dkt John Pombe Magufuli,Waziri Mkuu Kassim Majliwa na viongozi mbalimbali wa Kitaifa.
Imeelezwa kuwa ujio wa Waziri huyo Mkuu wa Ethiopia ni pamoja na kukuza mahusiano mazuri yaliyopo baina ya Tanzania na Ethiopia pamoja na kujadili fursa zaidi za ushirikiano katika maeneo mbalimbali ikiwemo uwekezaji na biashara.
Mhe. Dessalegn atakutana na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Joseph Magufuli kwa mazungumzo na kushuhudia uwekwaji saini wa mikataba ya ushirikiano kwenye maeneo mbalimbali kabla ya kuzungumza na Waandishi wa Habari.

Rais
Dkt John Pombe Magufuli akimpokea mgeni wake ,Waziri Mkuu wa Ethiopia
,Hailemariam Dessalegn,aliyewasili hivi punde katika uwanja wa ndege wa
Kimataifa wa Julius Nyerere,jijini Dar Es Salaam.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John
Pombe Magufuli akisalimiana na kumpokea mgeni wake Waziri Mkuu wa
Ethiopia Hailemariam Dessalegn mara baada ya kuwasili katika Uwanja wa
ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere Terminal One jijini Dar es Salaam.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John
Pombe Magufuli akiwa pamoja na mgeni wake Waziri Mkuu wa Ethiopia
Hailemariam Dessalegn mara baada ya kuwasili katika Uwanja wa ndege wa
Kimataifa wa Julius Nyerere Terminal One jijini Dar es Salaam.
Waziri Mkuu wa Ethiopia Hailemariam Dessalegn akipiga
ngoma mara baada ya kuwasili Ikulu jijini Dar es Salaam, Pembeni yake ni
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli
akimpigia makofi.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John
Pombe Magufuli akiwa na mgeni wake Waziri Mkuu wa Ethiopia Hailemariam
Dessalegn wakati nyimbo za mataifa mawili (Tanzania na Ethiopia) zikipigwa
mara baada ya kuwasili katika Uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Julius
Nyerere Terminal One jijini Dar es Salaam.
Waziri Mkuu wa Ethiopia Hailemariam Dessalegn akishuka
kwenye jukwaa kwenda kukagua gwaride la Heshma lililoandaliwa kwa ajili
yake.
Waziri Mkuu wa Ethiopia Hailemariam Dessalegn akikagua
Gwaride la heshma lililoandaliwa kwa ajili yake.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John
Pombe Magufuli akiwa katika mazungumzo na mgeni wake Waziri Mkuu wa
Ethiopia Hailemariam Dessalegn mara baada ya kuwasili Ikulu jijini Dar es
Salaam.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John
Pombe Magufuli akizungumza na wanahabari mara baada ya kumaliza
mkutano wa pamoja na Waziri Mkuu wa Ethiopia Hailemariam Dessalegn
aliyeambatana na ujumbe wake Ikulu jijini Dar es Salaam.
Waziri Mkuu wa Ethiopia Hailemariam Dessalegn akifurahia
jambo wakati Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe
Magufuli alipokuwa akizungumza na Wanahabari Ikulu jijini Dar es Salaam.
Waziri Mkuu wa Ethiopia Hailemariam Dessalegn
akizungumza na Wanahabari Ikulu jijini Dar es Salaam mara baada ya
mkutano wake na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John
Pombe Magufuli.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John
Pombe Magufuli akimtambulisha Katibu Mkuu Kiongozi Balozi Eng. John
Kijazi kwa mgeni wake Waziri Mkuu wa Ethiopia Hailemariam Dessalegn Ikulu
jijini Dar es Salaam.
Shamra shamra zikiendelea wakati wa kuwasili Waziri
Mkuu wa Ethiopia Hailemariam Dessalegn katika Uwanja wa ndege wa
Kimataifa wa Julius Nyerere Terminal 2 jijini Dar es Salaam.
Waziri Mkuu wa Ethiopia Hailemariam Dessalegn
akikaribishwa kwa kupewa ua na mtoto Xyleen Mapunda mara baada ya
kuwasili katika Uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere Terminal
One jijini Dar es Salaam. PICHA NA IKULU.
No comments:
Post a Comment