HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Friday, March 31, 2017

FIFA YABARIKI KUONGEZA TIMU HADI 48 KATIKA KOMBE LA DUNIA 2026



Chama cha soka duniani FIFA kimepanga kuwepo kwa michezo sita ili zipatikane timu zitakazoingia katika fainali za kombe la dunia mwaka 2020.

Rais wa shirikisho la soka Ulaya Aleksander Ceferin amesema kuwa amefurahishwa na hatua hiyo na nchi za Ulaya zitawakilishwa vyema.

FIFA imefafanua ni kwa namna gani timu 48 zitaweza kushiriki michuano hiyo na ila mwanachama wa FIFA atakuwa na uwezo wa kuongeza walau timu moja katika michuano ya mwaka 2026.

Mwenyeji wa fainali hizi ataingia moja kwa moja kama ilivyokua awali.



Mapendekezo hayo yapo hivi

Afrika - 9 kutoka timu za awali 5

Asia - 8 kutoka timu 4 za awali

Ulaya - 16 kutoka timu 13 za awali

Marekani ya Kaskazini, Kati na Caribbean - 6 kutoka timu 4 za awali

Bara la Oceania - 1 kutoka timu 1 ya awali

Amerika ya Kaskazini - 6 kutoka timu 4 za awali


Hatua ya nyongeza ya timu hizo inatajwa kama sababu mojawapo ya kuonekana kwa nchi ambazo zilikuwa hazipati nafasi


Mwezi januari chama hicho chenye mamlaka makubwa ya soka duniani, kilipanga kuongeza timu zitakazoshiriki michuano ya kombe la dunia kutoka 32 mpaka 48 na hii itaanza mwaka 2026.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad