HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Wednesday, March 1, 2017

NGOMA AWEKA WAZI MADUDU YA VIONGOZI WA YANGA


Na Mwandishi wetu, Dar es salaam.

MSHAMBULIAJI wa Yanga wa kimataifa kutoka nchini Mzimbabwe Donald Ngoma amesema ataondoka katika klabu hiyo kukwepa mambo ya ovyo ya uongozi.

Ngoma amesema hayo wakati akizungumzia tuhuma dhidi yake juu ya kutocheza mechi ya Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara dhidi ya Simba Jumamosi, Yanga ikichapwa mabao 2-1 Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.

Amesema kwamba ataondoka Yanga baada ya kuchoshwa na 'madudu' ya uongozi wa timu, mchezaji huyo amesema kwamba mashabiki na wapenzi wa Yanga wamekuwa wakimshutumu na kumtukana kutokana na taarifa zisizo za kweli zinazosambazwa kwenye mitandao ya kijamii kuhusu yeye. 
  
“Nimekuwa kimya wakati wote nikitukanwa juu ya sababu za kutocheza, wakati ukweli ni kwamba mimi nina maumivu ya goti. Taarifa nyingi zimekuwa zikisambazwa kwenye mitandao ya kijamii kwamba sitaki kucheza kwa sababu ninataka kuondoka katika timu, nashangaa wapi wanapata hizo taarifa,”amesema Ngoma.

Amesema Daktari ambaye Yanga walimtumia kumtibu yeye alikuwa ‘tapeli’ na ameilia fedha klabu bila kufanya kazi yoyote. “Daktari alikula fedha za viongozi wa klabu na kuwadanganya kwamba alikuwa ananitibu amenipeleka hospitali, wakati ukweli ni kwamba nilikuwa ninatibiwa katika hospitali nyingine kwa gharama zangu mwenyewe,”amesema Ngoma.

Mchezaji huyo mrefu mwenye nguvu na kasi uwanjani, amesema kwamba baadaye Daktari huyo alipoulizwa alisema kwamba niko fiti kucheza, wakati ukweli ni kwamba sikuwa tayari kabisa kucheza.

“Alikuwa anawaambia watu kwamba maumivu yangu yanaweza kupona ndani ya wiki mbili, wakati Daktari halisi aliyekuwa ananitibu alisema ninahitaji kati ya wiki sita hadi nane kupona. Tazama huyu Daktari feki alivyoleta mtafaruku kati yangu na timu,”amelalamika Ngoma.
Donald Dombo Ngoma anaelekea kukamilisha msimu wake wa pili tangu ajiunge na Yanga akitokea Platinums FC ya Zimbabwe mwaka 2015.

Ngoma ameweka wazima kuwa kwa sasa yeye na klabu wamefikia katika hatua ambayo atachukua maamuzi muda si mrefu na atatoa taarifa sahihi za kuondoka kwake kutokana na mambo ya ovyo ya viongozi wa klabu,”ameandika Ngoma katika akaunti yake ya Instagram leo asubuhi.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad