HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Saturday, March 11, 2017

MWENYEKITI WA CCM DKT MAGUFULI AONGOZA KIKAO CHA KAMATI KUU YA CCM LEO MJINI DODOMA

 Mwenyekiti wa CCM, Rais John Magufuli akipokewa na Katibu Mkuu wa CCM,Abdulrahman Kinana alipowasili Makao Makuu ya CCM, mjiniDodoma leo kuendesha kikao cha Kamati Kuu ya CCM.
 Mwenyekiti wa CCM, Rais Dk. John Maguguli akiwana Makamu Mwenyekiti wa CCM-Bara Philip Mangula (kushoto) kwenye chumba cha mapumziko kabla ya kuanza kikaocha Kamati Kuu ya CCM mjini Dodoma leo. Kulia ni Naibu Katibu Mkuu wa CCM-Zanzibar Vuai Ali Vuai na Makamu Mwenyekiti wa CCM, Rais wa Zanzibar Dk. Ali Mohamed Shein 
 Katibu Mkuu wa CCM, Abdulraman Kinana akishauriana jambo na Naibu Katibu Mkuu wa CCM Zanzibar Vuai Ali Vuai kabla ya kuanza kikao cha Kamati Kuu ya CCM mjini Dodoma leo. Kulia ni Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar, Balozi Seif Ali Idi
 Mwenyekiti wa CCM, Rais John Magufuli akiwa na viongozi wengine wa Chama wakati wakisubiri kuingia ukumbini kwenye kikao cha Kamati Kuu ya CCM,leo mjini Dodoma
 Baadhi ya Maofisa wa Chama wakiwa ukumbini wakati wa kikao hicho
 Wajumbe wa Kamati Kuu ya CCM, Stephen Wasira na William Lukuvi wakipitia makabrasha kabla ya kuanza kikao cha Kamati Kuu ya CCM mjini Dodoma leo
 Wajumbe wa Sekretarieti wakiwa ukumbi kusubiri kuanza kwa kikao cha Kamati Kuu ya CCM leo mjini Dodoma
 Wajumbe wa Kamati Kuu Jason Rweikiza (kushoto) na Alhaji Adan Kimbisa wakibadlishana mawazokabla ya kikao cha Kamati Kuu ya CCM kuanza mjini Dodoma leo
 Wajumbe wa Kamati Kuu ya CCM, Hussein Mwinyi na Jerry Silaa, wakibadilishana ma wazokabla ya kikao hicho kuanza

Wajumbe wa Kamati Kuu ya CCM, Alhaj Abdallah Bulembo na Shamsi Vuai Nahodha wakibadilishana mawazo kabla ya kikao hicho kuanza leo mjini Dodoma.

 Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana akiingia ukumbini
 Mwenyekiti wa CCM Rais Dk. John Magufuli akiwasili ukumbini kuendesha kikao cha Kamati Kuu ya CCM mjini Dodoma leo. Kushoto ni Makamu Mwenyekiti wa CCM-Rais wa Zanzibar Dk. Ali Mohammed Shein na kulia ni Makamu Mwenyekiti wa CCM Bara PhilipMangula na Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana

Naibu Katibu Mkuu wa CCM-Bara, Rodrick Mpogolo akisalimiana na Spika wa Baraza la Wawakilishi Zanzibar, Zubeir Ali Maulidikabla ya kuanza kikao hicho. Katikati ni Spika wa Bunge Job Ndugai

 Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana akitoa utangulizi kumpa nafasi Mwenyekiti wa CCM, Rais Dk JohnMagufulikufungua na kuongoza kikaocha Kamati Kuu ya CCM leo mjini Dodoma. Kushoto ni Dk. Shein na Kulia ni Mangula.

Makamu wa Rais Samia Suluhu Hassan akiwa kwenye kikao hicho. Kushoto ni Katibu wa NEC, Oganaizesheni Mohamed Seif Khatib na Naibu Katibu Mkuu wa CCM Zanzibar Vuai Ali Vuai

 Mwenyekiti wa CCM,Rais Dk John Magufuli akiendesha kikao cha Kamati Kuu ya CCM leo mjini Dodoma
 Mwenyekiti wa CCM, Rais Dk John Magufuli na viongozi wenzake wa meza kuu, wakifurahia jambo wakati wa kikao hicho cha Kamati Kuu ya CCM leo mjini Dodoma. (Picha zote na Bashir Nkoromo)

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad