HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Saturday, March 11, 2017

Diwani Saidi Fella apokea Msaada kutoka Oxford

Diwani wa Kata ya Kilungule Mh. Saidi Fella leo amepokea msaada wa vitabu vya kufundishia na  kujifunzia kwa wanafuzi wa shule za msingi pamoja na Sekondary kutoka kwa rafiki zake wa Oxford University Press Tanzania, Vitabu hivyo vimegawiwa katika shule ya msingi Charambe, Chemchem pamoja na Kingugi na kwa upande wa Sekondary ni Charambe na

Diwani Saidi Fella amewashukuru Oxford na kuwasisitiza wanafunzi kusoma kwabidii kupitia vitabu lakini pia kuvitunza kwa maana ya wadogo zao kuju kuvitumia vitabu hivyo kwa baadae, hata hivyo amewata walimu kuhakikisha wanavipiga mihuri vitabu ili wanafunzi wanapo azima kwenda kusoma nyumbani wakumbuke kuvirejesha.

Maria Mlay kutoka Oxford amewasisitiza wanafunzi kusoma kwa bidii kupitia vitabu hivyo ili kutimiza ndoto zao katika maisha lakini pia kuvitunza vitabu hivyo.
Aidha Saidi Fella amewashukuru Oxford kwa mchango huo wa vitabu katika kata yake na ameendelea kusisitiza wadua kuendelea kumsapoti katika kata yake ya Kilungule kwani ni Kata mpya na bado inamaitaji mengi zaidi ya miundo mbinu, Afya pamoja na Elimu.


Picha ya Pamoja wanafunzi na walimu baada ya kupokea vitabu





No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad