HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Thursday, March 16, 2017

AHMAD AHMAD AMBWAGA ISSA HAYOTOU UCHAGUZI WA CAF

Rais Shirikisho la Mpira wa Miguu Barani Afrika (CAF) Ahmad Ahmad kutoka nchini Madagascar


Uchaguzi wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Barani Afrika (CAF) umemalizika kwa mgombea Ahmad Ahmad kutoka nchini Madagascar kupata kura 34 dhidi ya 20 za aliyekuwa rais wa zamani Issa Hayatou uliofanyika leo nchini Ethiopia.

Uchaguzi huo uliokuwa na ushindani mkubwa kutoka kwa pande zote uliweza kuhitimishwa na wanachama washiriki kutoka nchi mbalimbali barani Afrika kupiga kura za kumchagua ni nanai atakayeongoza shirikisho hilo kwa kipindi kijacho.

Pamoja na uchaguzi huo, CAF wameweza kuipitisha Zanzibar kuwa mwanachama rasmi ambapo kwa sasa atakuwa mshiriki rasmi wa michuano ya kimataifa iliyo chini ya CAF pamoja na kuwa na timu ya Taifa inayojitegemea.

Nchi takribani zote ziliweza kukubali kupatiwa kwa uanachama huo na nchi 51 kukubali na 3 kukataa ambazo ni Benini, Sychells na Madagascar.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad