HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Saturday, February 25, 2017

RAIS WA UGANDA YOWERI MUSEVENI AWASILI NCHINI NA KUPOKELEWA NA MWENYEJI WAKE RAIS DKT JOHN POMBE MAGUFULI


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwa na mgeni wake Rais wa Uganda,Yoweri Kaguta Museveni baada ya kuwasili katika uwanja wa ndege wa Kimataija wa Julius Nyerere,jijini Dar es Salaam.
Rais wa Uganda,Yoweri Kaguta Museveni akikagua gwaride la heshima mara baada ya kuwasili katika uwanja wa ndege wa kimataifa wa Julius Nyerere,jijini Dar.

Makamu wa Rais Mama Samia akimkaribisha Rais wa Uganda,Yoweri Museveni mara baada ya kuwasili uwanja wa ndege mapema leo kwa ziara ya siku mbili,anaeshuhudia pichani kati ni Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,Dkt John Pombe Magufuli


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwa na mgeni wake Rais wa Uganda,Yoweri Kaguta Museveni wakiwa wamesimama wakati wa nyimbo za Taifa zikipigwa.

Makamu wa Rais Mama Samia Suluhu Hassan,Waziri Mkuu Kassim Majaliwa na Waziri wa Mambo ya Nje na ushirikiano wa Afrika Masharika,Dkt Augustine Mahiga kwa pamoja wakiwa tayari kumpokea mgeni wao,Rais wa Uganda Yoweri Museveni
Baadhi ya wageni waalikwa mbalimbali waliofika uwanja wa Ndege kumlaki Rais wa Uganda,Yoweri Museveni

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwa na mgeni wake Rais wa Uganda,Yoweri Kaguta Museveni wakifurahia vikundi vya ngoma za asili vilivyokuwa vikiburudisha mara baada ya Rais huyo kuwasili. 

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad