Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini, Profesa Justin Ntalikwa (kulia) na Mwakilishi wa Waziri Mkuu wa Uingereza anayehusika na masuala ya Biashara nchini Kenya na Tanzania, Lord Hollick wakimsikiliza mmoja wa Wataalam wa Wizara ya Nishati na Madini (hayupo pichani) wakati wa kikao kilichofanyika katika Ofisi za Wizara ya Nishati na Madini jijini Dar es Salaam.
Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini, Profesa Justin Ntalikwa (kulia) akimsikiliza Balozi wa Uingereza nchini Tanzania Sarah Cooke, (kushoto) aliyeambatana Mwakilishi wa Waziri Mkuu wa Uingereza anayehusika na masuala ya Biashara nchini Kenya na Tanzania, Lord Hollick (katikati). kikao kilifanyika katika Ofisi za Wizara ya Nishati na Madini jijini Dar es Salaam.
Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini, Profesa Justin Ntalikwa (katikati) akiongoza kikao baina ya Ujumbe kutoka nchini Uingereza ukiongozwa na Balozi wa Uingereza nchini Tanzania Sarah Cooke pamoja Watendaji mbalimbali wa Idara ya Nishati katika Wizara ya Nishati na Madini.
Na Teresia Mhagama, Dar es Salaam
Katibu
Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini, Profesa Justin Ntalikwa tarehe 16
Februari, 2017 amekutana na Ujumbe
kutoka Ubalozi wa Uingereza nchini Tanzania ukiongozwa na Balozi, Sarah Cooke, aliyeambatana na Mwakilishi wa Waziri Mkuu wa Uingereza anayehusika na
masuala ya Biashara nchini Kenya na Tanzania, Lord Hollick na Mshauri wa Hali ya Hewa na
Mazingira.
Katika
kikao hicho walijadili masuala mbalimbali ikiwemo upunguzaji wa madeni ya
Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) ili Shirika hilo liweze kujiendesha lenyewe
kwa ufanisi pamoja uendelezaji wa miradi ya uzalishaji, usafirishaji na
usambazaji wa umeme.
Profesa
Ntalikwa pia aliueleza Ujumbe huo kuhusu mipango inayofanywa na Serikali ya
kuendeleza miradi mbalimbali ya umeme ikiwemo uandaaji wa kabrasha litakaloainisha miradi yote ya umeme inayohitaji wawekezaji.
Alisema
kuwa kabrasha hilo litasambazwa kwa wadau mbalimbali na wawekezaji ili waweze
kulisoma na kufanya maamuzi ya kuwekeza kwenye miradi husika.
“Kabrasha
hilo limeshaandaliwa na Wataalam na kwa sasa linapitiwa na baadhi ya Taasisi za
Serikali kabla ya kulisambaza kwa wadau
wetu kupitia njia mbalimbali kama Tovuti na magazeti,” alisema Profesa
Ntalikwa.
Kwa
upande wake, Mwakilishi wa Waziri Mkuu wa Uingereza anayehusika na
masuala ya Biashara nchini Tanzania,
Lord Hollick alisema kuwa kipaumbele cha nchi hiyo ni kuwekeza kwenye
miradi ya nishati kwani Tanzania ina vyanzo vingi vya nishati jadidifu ikiwamo, Jotoardhi, maporomoko madogo ya Maji,
Tungamotaka, Jua na Upepo.
“
Tunao mtaji wa kuwekeza kwenye miradi ya umeme na pia tunaweza kusaidia
kiutaalam ili kuifanya TANESCO kufanya kazi kwa ufanisi ili kupunguza
changamoto mbalimbali zinazochelesha uwekezaji,” alisema Hollick.
No comments:
Post a Comment