HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Monday, February 20, 2017

MAJALIWA AFANYA ZIARA BABATI NA MBULU

 Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akitazama sukari na nishati ya kuni inayotengenezwa kwa kutumia makapi ya miwa inayokamuliwa katika kiwanda cha sukari cha Manyara wakati alipotembelea kiwanda hicho Februari 19, 2017.  Kuni hizo zina ubora unaofanana na ule wa makaa ya mawe na hutumika zaidi katika mitambo inayotumia  nishati ya kuni. Kulia ni Waziri wa  Kilimo, Mifugo na Uvuvi, Dkt. Charles Tizeba na kulia kwa Waziri Mkuu, ni Mkuu wa Mkoa wa Manyara, Dkt. Joel Bendera. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
 Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akisalimiana na Mkuu wa wilaya mstaafa, Mama Sanka baada  ya kuwasili  kwenye makazi ya Mkuu wa Mkoa wa Manyara  mjini Babati akiwa katika ziara ya mkoa huo, Februari 19, 2017.
 Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akitazama sanamu ya binadamu  wakati alipotembelea moja ya darasa  la Chuo cha Uuguzi katika hospitali ya Haydom wilayani Mbulu, Februari 20, 2017.
 Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa  akipata maelezo kutoka kwa Mtafiti katika hospitali ya Haydom wilayani Mbulu, Rosemary Mshama  (kulia)  wakati alipotembelea Kituo cha Utafiti cha hospitali hiyo Februari 20, 2017. 
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akifurahia ngoma ya asili ya kabila la Wahatzabe wakati alipowasili kwenye hospitali ya Haydom kuanza ziara ya  wilaya ya Mbulu, Februari 20, 2017. 

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad