HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Friday, February 10, 2017

KUKOSEKANA KWA HUDUMA YA MAJISAFI KATIKA MAENEO YA MAKONGO JUU NA GOBA

Shirika la Maji Safi na Majitaka Dar-es-salaam (DAWASCO), linawatangazia wakazi wa Maeneo ya Makongo na Goba jijini Dar es Salaam kuwa kuna tatizo la upatikanaji wa huduma ya Maji katika maeneo tajwa hapo juu, kuanzia siku ya Alhamisi tarehe 09/02/2017.

Sababu ya kukosekana kwa huduma ya Maji inatokana na hitilafu ya Pampu ya kusukuma Maji .Mafundi wetu wanaendelea na jitihada ili kuhakikisha huduma ya Maji inarejea.

Maeneo yaliyoathirika na hitilafu hii ni Goba Kunguru, Goda Kinzudi, Makongo Juu yote, Mbezi Juu eneo la Baraza la Mitihani na Eneo la Mnara wa Voda.

DAWASCO INAOMBA RADHI WANANCHI WA MAENEO HUSIKA KWA USUMBUFU UTAKAOJITOKEZA.

Kwa taarifa zaidi wasiliana nasi kupitia kituo cha huduma kwa wateja 0800110064 (BURE), Pamoja na Dawati la huduma kwa Mteja DAWASCO  Mkoa wa Kawe 0743-451861.

IMETOLEWA NA:
OFISI YA UHUSIANO
DAWASCO-MAKAO MAKUU

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad