HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Friday, February 17, 2017

AHUKUMIWA KWENDA JELA MIAKA 20, KWA KUMBAKA MWANAE NA KUMSABABISHIA ULEMAVU CHUNYA MKONI MBEYA.

Hakimu mkazi wa Wilaya ya Chunya Desdery Magezi amemhukumu kwenda jela miaka ishirini na viboko nane Maneno Pesambili Kanjanja au Maneno Pesambili Lyimo(59)mkazi wa kijiji cha Kiwanja Kata ya Mbugani Wilaya ya Chunya baada ya kumkuta na hatia ya kumwingilia kimwili binti yake mwenye umri wa miaka 19 na kumfungia ndani kwa miaka miwili na kumnyima haki za msingi kama chakula na kisha kumsababishia ulemavu wa miguu kwa kushindwa kutembea.https://lh3.googleusercontent.com/-hBkrT2YVo5I/WKawbtCx52I/AAAAAAAAFHk/y5dtrjZ5mRY/%25255BUNSET%25255D.jpg
Mwendesha mashitaka wa Serikali Frederick Ndosi amesema kuwa kosa hilo ni kinyume cha sheria namba 158 (1)b sura ya 16 iliyopitiwa mwaka 2002 ambapo mshitakiwa amedaiwa kutenda kosa hilo katika vipindi tofauti kati ya 2015 hadi 23 Januari mwaka alipokamatwa na kufikishwa mahakamani januari 30 mwaka huu. Upande wa mashitaka ulileta mashahidi watano akiwemo mtoto aliyefanyiwa ukatili na mahakama kuridhika pasipo shaka na ushahidi wake. 
Hata hivyo Ndosi aliiomba mahakama kutoa adhabu kali kwa mshitakiwa ili iwe fundisho kwake na wengine wenye kufanya vitendo vivyo. Akijitetea mbele ya Mahakama Maneno amesema kuwa kesi hiyo imetengenezwa ili kumtia hatiani hivyo mahakama imuonee huruma kwa kuwa hakutenda kosa hilo. Baada ya Hakimu Magezi kusikiliza pande zote mbili mbili alimtia hatiani mshitakiwa na kumtaka kwenda jela miaka ishirini na viboko nane ili kutengwa na jamii. 
Nje ya Mahakama binti aliyetendewa ukatili huo amesema kuwa adhabu hiyo ni ndogo hata kama ni Mzazi wake na anajisikia vibaya anapokumbuka tukio hilo na kuamua kubadilisha jina na sasa kuitwa Mariam Maneno. 
Aidha amewashukuru wasamaria wema ambao wanaendelea kumhifadhi akiwemo mkuu wa Wilaya ya Chunya Rehema Madusa.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad