
Kama unaishi au ulikuwa na mpango wa kuja kutafuta maisha jijini Dar es Salaam, Jumia Travel inakushauri kujaribu kufanya shughuli zifuatazo ili kukuingizia kipato:
Kuuza vinywaji baridi (maji, soda, juisi, n.k.)
Kwa kipindi kirefu hali ya hewa ya jiji la Dar es Salaam huwa ni joto na jua kali, hivyo kupelekea uhitaji na utumiaji mkubwa wa vinywaji baridi. Hii ni fursa kubwa kwa wafanyabiashara kwani watu hawawezi kuvumilia jua kali bila ya kutumia vinywaji kama vile maji, soda au juisi. Mtaji wa biashara hii sio mkubwa sana na haihitaji ofisi, kitu ambacho kinamuwezesha mtu yeyote kufanya biashara hii.
Kwa kipindi kirefu hali ya hewa ya jiji la Dar es Salaam huwa ni joto na jua kali, hivyo kupelekea uhitaji na utumiaji mkubwa wa vinywaji baridi. Hii ni fursa kubwa kwa wafanyabiashara kwani watu hawawezi kuvumilia jua kali bila ya kutumia vinywaji kama vile maji, soda au juisi. Mtaji wa biashara hii sio mkubwa sana na haihitaji ofisi, kitu ambacho kinamuwezesha mtu yeyote kufanya biashara hii.

Kuuza matunda
Wakazi wa jiji hili hupendelea matunda katika milo yao tofauti iwe ni asubuhi, mchana au usiku. Biashara hii ni nzuri kwa kigezo kikubwa kwamba watu hawana mashamba, matunda mengi huingizwa kutoka mikoa mingine. Mtaji wa biashara hii ni mdogo na sehemu nzuri za kupatia wateja ni kwenye vituo vya mabasi, pembezoni mwa barabara, karibu na migahawa au karibu na ofisi.
Wakazi wa jiji hili hupendelea matunda katika milo yao tofauti iwe ni asubuhi, mchana au usiku. Biashara hii ni nzuri kwa kigezo kikubwa kwamba watu hawana mashamba, matunda mengi huingizwa kutoka mikoa mingine. Mtaji wa biashara hii ni mdogo na sehemu nzuri za kupatia wateja ni kwenye vituo vya mabasi, pembezoni mwa barabara, karibu na migahawa au karibu na ofisi.
Kuuza magazeti
Magazeti ni nyenzo mojawapo ya kupatia habari ambayo wakazi wengi wa Dar es Salaam huitumia. Kutokana na kutingwa na shughuli nyingi, wengi wao huwa hawana muda wa kupitia kwenye sehemu maalum zinazouza magazeti. Njia pekee ya kuwafikia ni kwenye foleni za magari asubuhi wanapokwenda na jioni wanaporudi kwenye shughuli zao.
Uchuuzi wa vyakula vya baharini (Pweza, ngisi, dagaa kamba, n.k.)
Kuuza vocha za muda wa maongezi wa kwenye simu
Faida ya kuishi kwenye jiji hili ni kwamba makampuni na taasisi zote kubwa ofisi zake zinapatikana hapa. Hali hiyo hutoa fursa kwa wafanyabiashara kuwa mawakala ili kuwafikia wateja wa kawaida. Mojawapo ya huduma muhimu inayotumika muda wote ni huduma za simu za mkononi kwa ajili ya mawasiliano ambapo si chini ya makampuni matano yanaendesha shughuli zake. Hii hupelekea wanaouza vocha za muda wa maongezi kuwa na uhakika na biashara zao.

No comments:
Post a Comment