HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Tuesday, January 31, 2017

WAZIRI MWAKYEMBE AKABIDHI TUZO ZA RITA KWA VIONGOZI WA MIKOA YA IRINGA NA NJOMBE KWA KUFANIKISHA USAJILI NA KUTOA VYETI VYA KUZALIWA KWA WATOTO

Waziri wa Mambo ya Katiba na Sheria Mhe. Dr. Harrison Mwakyembe amekabidhi Tuzo na Hati za Pongezi kwa Viongozi wa Mikoa ya Iringa na Njombe kwa kufaikisha na kutekeleza kikamilifu Mpango wa Usajili na kutoa Vyeti vya Kuzaliwa kwa Watoto walio na Umri chini ya Miaka Mitano uliozinduliwa katika Mikoa hiyo tarehe 22 Septemba 2016. 

Tuzo hizo zimetolewa kwa Halmashauri 11 za Wilaya na Miji, Ofisi za Wakuu wa Wilaya 7 na Ofisi za Wakuu wa Mikoa 2 kwa kuweza kusajili na kuwapa vyeti vya kuzaliwa kwa asilimia 100 hivyo kuvuka lengo lililokuwa limewekwa. Usajili kupitia mfumo huu ulifanyika kwa kutumia Ofisi za Watendaji Kata na Vituo vya Tiba vinavyotoa Huduma ya afya ya mama na mtoto. Hafla ya kukabidhi tuzo ilifanyika katika Ukumbi wa Chuo cha Maendeleo ya Jamii Njombe.
Waziri wa Mambo ya Katiba na Sheria Mhe. Dkt. Harrison Mwakyembe (waliokaa katikati) akiwa katika picha ya pamoja na viongozi wa Mikoa ya Iringa na Njombe mara baada ya kukabidhi tuzo za pongezi kwa kufanikisha Mpango wa Usajili na Kutoa Vyeti vya kuzaliwa kwa watoto. Viongozi wengine (waliokaa) kuanzia kulia ni Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu kanda ya Iringa Mhe. Mary Shangali, Mkuu wa Mkoa wa Iringa Mhe. Amina Masenza, Mkuu wa Mkoa wa Njombe Mhe. Christopher Ole Sendeka na Kaimu Afisa Mtendaji Mkuu wa RITA, Bi. Emmy Hudson. Waliosimama ni Wakuu wa Wilaya wa Mkoa wa Iringa na Njombe.
Waziri wa Mambo ya Katiba na Sheria Mhe. Dr. Harrison Mwakyembe amekabidhi Tuzo na Hati za Pongezi kwa Viongozi wa Mikoa ya Iringa na Njombe kwa kufaikisha na kutekeleza kikamilifu Mpango wa Usajili na kutoa Vyeti vya Kuzaliwa kwa Watoto walio na Umri chini ya Miaka Mitano uliozinduliwa katika Mikoa hiyo tarehe 22 Septemba 2016. Tuzo hizo zimetolewa kwa Halmashauri 11 za Wilaya na Miji, Ofisi za Wakuu wa Wilaya 7 na Ofisi za Wakuu wa Mikoa 2 kwa kuweza kusajili na kuwapa vyeti vya kuzaliwa kwa asilimia 100 hivyo kuvuka lengo lililokuwa limewekwa. Usajili kupitia mfumo huu ulifanyika kwa kutumia Ofisi za Watendaji Kata na Vituo vya Tiba vinavyotoa Huduma ya afya ya mama na mtoto. Hafla ya kukabidhi tuzo ilifanyika katika Ukumbi wa Chuo cha Maendeleo ya Jamii Njombe.
Mkuu wa Mkoa wa Njombe Mhe. Christopher Ole Sendeka akionesha tuzo aliyokabidhiwa kutokana na Mkoa wake kufanikisha kusajili watoto kwa asilimia mia moja. Wengine katika picha ni Waziri wa Mambo ya Katiba na Sheria Mhe. Dkt. Harrison Mwakyembe (Katikati) na Mkuu wa Mkoa wa Iringa Mhe. Amina Masenza.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad