HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Monday, January 23, 2017

Rais Donald Trump awafuta kazi mabalozi wote wanaiwakilisha Marekani duniani

Rais wa Marekani Donald Trump amewafuta kazi mabalozi wote wa nchi hiyo kote duniani na wanaohudumu katika mashirika ya kimataifa.
Kwa mujibu wa taarifa ya mtandao wa Independent, mabalozi hao wametakiwa kuachia nafasi zao mara moja na kurudi nyumbani.
Kiongozi huyo juzi alifanya ziara yake ya kwanza katika ofisi za makao makuu ya shirika la Ujasusi la Marekani CIA, na kuvituhumu baadhi ya vyombo vya habari nchini humo wakati akitoa hotuba yake, kwamba vinawagawa wananchi.
Zaidi ya mabalozi 80 wa Marekani katika nchi mbali mbali duniani walifutwa kazi Ijumaa tarehe 20 Disemba saa sita mchana punde baada ya Trump kuapishwa.
Hatua hiyo ya Trump inatazamiwa kuvuruga uhusiano na waitifaki muhimu kama vile Ujerumani, Uingereza, Canada. Inatabiriwa kuwa nchi hizo zinaweza kukaa bila mabalozi kwa miezi kadhaa kwani baada ya Trump kuteua mabalozi wapya watalazimika kuidhinishwa na Bunge la Kongresi kabla ya kuanza kazi zao.

Source: Independent

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad