HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Saturday, January 21, 2017

RAIS DONALD TRUMP AANZA KUISHUGHULIKIA SHERIA YA OBAMACARE

Rais wa Marekani Donald Trump amechukua hatua ya kwanza akiwa madarakani, kutia saini agizo lake la kutaka kufanyiwa mabadiliko ya sera ya matibabu ya rais aliyemaliza muda wake Barack Obama.

Agizo hilo la rais Trump, limeziagiza taasisi husika kuangalia namna ya kupunguza mzigo wa kiuchumi uliosababishwa na sheria ya matibabu, inayojulikana zaidi nchini humo kama Obamacare.

Akiapishwa jana rais Trump, aliahidi kuanzia jana kuwa ataweka maslahi ya Marekani kwanza, kufufua viwanda na kujenga miundombinu ya Marekani ambayo amesema imeoza na kutelekezwa.

Baadaye leo kundi la wanawake 200,000 wameahidi kushiriki maandamano ya Wanawake Jijini Washington, ambayo waandaji wamesema yanalenga kuangazia ubaguzi na suala la usawa ambalo linakabiliwa na tishio chini ya utawala wa Trump.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad