HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Thursday, January 12, 2017

MAKOCHA SIMBA, AZAM WATAMBIANA FAINALI MAPINDUZI CUP KESHO

Kocha  msaidizi wa Simba Jackson Mayanja

Na Zainab Nyamka, Globu ya Jamii
Kueleka mchezo wa fainali wa kombe la Mapinduzi baina ya Azam na Simba makocha wa pande zote mbili wameanza kutambiana kila mmoja akijinadi kuwa ana uwezo wa kumfunga mwenzake ndani ya dakiika 90.
Fainali hiyo inayofanyika kesho kwenye uwan ja wa Amani inawakutanisha timu hizo zilizofanikiwa kuingia hatua hiyo Azam wakiwatoa Jang'ombe Taifa kwa goli 1-0, Simba wakiwatoa Yanga kwa mikwaju ya penati 4-2.
Kocha  msaidizi wa Simba Jackson Mayanja amejigamba kwa kusema kuwa mechi kati yao na Azam ni mechi ya fainali na ina utofauti mkubwa sana na mchezo uliopita wa watani wao wa jadi na walifanikiwa kuwaondoa kwa mikwaju ya penati.
Ameweka wazi kuwa mechi hiyo itarajiwa kuwa ni moja ya mchezo wa kukata na shoka kwani silaha zoet zipo kamili na zinajiandaa kikamilifu kabisa. “Maandalizi yapo vizuri kabisa, tuna majeruhi wawili ambao ni Blagnon pamoja na Mohamed Ibrahim kwani hatuna uhakika kama anaweza kucheza ila  wengine wote wako vizuri,”
Kocha wa muda wa Azam Idd Cheche amesema kuwa wachezaji wake wapo tayari kupambana na anataka kuhakikisha analichukua kombe la Mapinduzi kwani timu nzima inajiamini na watashuka dimbani kupambana. Pia amesifu safu yake ya ushambuliaji kutokuruhus goli hata moja mpaka wanaingia  hatua ya fainali ya Mapinduzi Cup 2017.
Cheche amejigamba kuwa anaifahamu vizuri Simba toka anacheza na pia amecheza nazo nikiwa mchezaji na sasa hivi ni mwalimu najua najua jinsi ya kuzikamata.
Azam imelichukua kombe la Mapinduzi mara mbili (2012 na 2015) tangu ilipoanza kushiriki michuano hiyo wakati Simba tangu 2007 wamelibeba mara tatu (2008, 2011 na 2015)

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad