HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Monday, January 30, 2017

BODI YA WAKURUGENZI DCB WAIPONGEZA TAWI LA MAGOMENI KWA KUFANYA VIZURI 2016.

Na Zainab Nyamka, Globu ya Jamii

BENKI ya DCB wamewazawadia tuzo tawi la Magomeni inayojulikana kama Chairman's awards baada ya kufanya vyema kiutendaji na kuwapiku matawi mengine ya benki hiyo na kutakiwa kuendelea kudumisha  ufanisi wa kazi.

Akizungumza kabla ya kutangaza kwa mshindi, Mkurugenzi Mtendaji wa DCB Edmund Mkwawa alisema kuwa matawi ya benki hupimwa kwa kutekeleza viashiria mbalimbali ikiwemo ukuaji wa amana zitokanazo na akaunti za hundi na akiba kwa asilimia 15, utoaji wa mikopo kwa asilimia 15, faida kabla ya kodi, ufuatiliaji wa mikopo chechefu na asilimia ya mikopo chechefu.

Mkwawa alisema kuwa, ili mshindi aweze kutangazwa ni lazima tawi husika kufikisha alama 60 ambzo zitagawiwa katika kutekeleza viashiria 10 na shindano hili lilianza toka Oktoba 2011 na tawi la Tabata ndilo lilikuwa la kwanza kuanza kuchukua tuzo hiyo.

Mbali na hilo, benki hiyo iliweza kutoa zawadi kwa meneja wa mikopo kwa vikundi kiasi cha shillingi laki tano (500,000), wasimamizi 9 wa mikopo kutoka matawi yoye kila mmoja akizawadiwa shilingi laki tatu (300,000) na maafisa watano kila mmoja shilingi laki mbili (200,000) ikiwa na lengo la kuwapatia motisha ya kufanya kazi kwa bidii zaidi na kusimamia vizuri uendeshaji wa mikopo hiyo.

Makamau Mwenyekiti wa bodi hiyo, Lucian Msambichaka amewapongeza tawi la Magomeni kwa jitihada kubwa walizozionyesha na kuwataka kuendelea kufanya vizuri zaidi na kuwasisitiza kuongeza ufanisi wa kibiashara kwa kuleta changamoto ya kushindanisha matawi hayo katika kila nyanja za huduma za kibenki.
  Mkurugenzi Mtendaji wa DCB Edmund Mkwawa akizungumza wakati wa utoaji wa tuzo kwa tawi la Magomeni baada ya kufanya vyema kiutendaji na kuwapiku matawi mengine ya benki hiyo na kutakiwa kuendelea kudumisha  ufanisi wa kazi.
Makamu Mwenyekiti wa bodi ya DCB Lucian Msambichaka akizungumza wakati wa utoaji wa tuzo kwa tawi  la Magomeni baada ya kufanya vyema kiutendaji na kuwapiku matawi mengine ya benki hiyo na kutakiwa kuendelea kudumisha  ufanisi wa kazi.
 Makamau Mwenyekiti wa bodi ya DCB Lucian Msambichaka akikabudhi zawadi kwa  na maafisa watano kila mmoja shilingi laki mbili (200,000) ikiwa na lengo la kuwapatia motisha ya kufanya kazi kwa bidii zaidi na kusimamia vizuri uendeshaji wa mikopo hiyo.
Makamu Mwenyekiti wa bodi ya DCB Lucian Msambichakana (wa pili kutoka kulia)akitoa zawadi ya mfano wa hundi kwa maafisa tisa  kila mmoja shilingi laki tatu(300,000) ikiwa na lengo la kuwapatia motisha ya kufanya kazi kwa bidii zaidi na kusimamia vizuri uendeshaji wa mikopo hiyo.

Makamu Mwenyekiti wa bodi ya DCB Lucian Msambichakana (wa pili kutoka kulia) akimkabidhi  Meneja wa Mikopo ya vikundi Maria Kabeho mfano wa hundi wa shilingi laki tano (500,000) akishuhudiwa na  Mkurugenzi Mtendaji wa DCB Edmund Mkwawa pamoja na wajumbe wa bodi hiyo Maharage Chande na Stephen Mulisa.
 Makamu Mwenyekiti wa bodi ya DCB Lucian Msambichakana akimkabidhi alyekuwa meneja mwandamizi wa tawi la Magomeni Gray Ndandika tuzo ya Chairman's awards baada ya kuibuka kidedea.
Wafanyakazi wa tawi la Magomeni wakiwa katika picha ya pamoja na Makamu Mwenyekiti wa bodi ya DCB Lucian Msambichakana,  Mkurugenzi Mtendaji wa DCB Edmund Mkwawa pamoja nawajumbe wa bodi hiyo Maharage Chande na Stephen Mulisa.
  Washindi mbalimbali wakiwa katika picha ya pamoja na Makamu Mwenyekiti wa bodi ya DCB Lucian Msambichakana, Mkurugenzi Mtendaji wa DCB Edmund Mkwawa pamoja na wajumbe wa bodi hiyo Maharage Chande na Stephen Mulisa.
 Wafanyakaiz wa Magomeni wakiwa wanashangilia ushindi baada ya kutangazwa.
Makamu Mwenyekiti wa bodi ya DCB Lucian Msambichakana (wa pili kutoka kushoto) akipiga makofi sambamba na Mkurugenzi Mtendaji wa DCB Edmund Mkwawa pamoja na  wajumbe wa bodi hiyo Maharage Chande na Stephen Mulisa. Picha na Zainab Nyamka.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad