HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Saturday, December 10, 2016

WATANZANIA WAASWA KUHURUMIANA NA KUPENDANA BILA KUJALI ITIKADI ZA DINI

Shekhe Hemed Jalala  akizungumza na waandishi wa habari kuelekea maadhimisho ya Siku ya kuzaliwa Mtume ( S.A.W), kulia ni mlezi wa Hauzat  Imamu Swadiq Mzee Rashidi  Mashtog na  upande wa kushoto ni  Naibu kiongozi Mkuu Mohammad Abdi .


Na Anthon John Globu ya jamii
IKIWA  imesalia siku moja kufikia maadhimisho ya kuzaliwa Mtume Muhammad Kiongozi wa waislam wa madhebu ya shia Ithnashariya  Tanzania  Shekhe Hemed  Jalala amewataka  watanzania kuwa na tabia ya kuhurumiana hasa wenye uwezo kuwahurumia wasio na uwezo.

Akizungumza na waandishi wahabari Leo katika ukumbi wa habari maelezo Jijini Dar es salaam amesema Mtume Mohammad alifundisha kuwa dini imekuja kutunza Upendo na amani hivyo ni vyema waTanzania  kuishi kwa Upendo bila kujali utofauti wa dini zao.
  
"Mtu kupenda nchi ni katika amani na pia dini imekuja kutunza upando na amani watanzania tusibaguane kutokana na dini zetu" amesema Jalala.

Hata Hivyo Sheikh Hemed amebainisha kuwa ni vyema jamii kuyaishi maisha aliyoishi Mtume Mohammad ikiwa ni pamoja na sifa kuumbili alizokuwa nazo Mtume ambazo  nikuwa mkweli na mwaminifu.
  
Sambamba na hayo ameongeza kuwa Kazi kubwa inayotakiwa kufanywa na watanzania hasa kwa kipindi hiki chakukumbukwa kwa kuzaliwa kwa Mtume ni kuishi kwa amani na ushirikiano kwa kuwa vitabu vyote vya dini vimekuja kuunganisha watu.                        

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad