HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Thursday, December 8, 2016

UDART KUENDELEA KUTOA HUDUMA BOARA USAFIRI KWA JIJI LA DAR ES SALAAM

Afisa Mawasiliano wa Udart, Deus Buganywa akizungumza na waandishi habari hawapo pichani juu ya utoaji huduma ya usafiri katika jiji la Dar es Salaam, leo.
Abiria wakiwa katika Kituo cha mabasi yaendayo Haraka leo jijini Dar es Salaam.picha na Emmanuel Massaka,Globu ya Jamii.

Na Chalila Kibuda, Globu ya Jamii
Kampuni ya usafiri katika jiji la Dar es Salaam (UDART) imesema kuwa litaendelea kutoa huduma bora ya usafiri kadri ya uwezo wao.

Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam, Afisa Mawasiliano wa Udart , Deus Buganywa amesema nia ya kampuni ni kuona wananchi wa jiji la Dar es Salaam wanapata huduma usafiri ulio bora.

Deus amesema kampuni imekuwa ikipokea maoni mbalimbali ya wananchi na kuweza kufanyia kazi katika masuala ua utoaji huduma ya usafiri.

Amesema abiria ni kiungo kikubwa kwao katika kuwasafirisha kutoka sehemu moja na kwenda nyingine bila usumbufu huku mifumo mingine ikiendeleaa kuimarishwa ukiwemo wa matumizi ya kadi.

Aidha amesema wanafunzi sasa wamekuwa na usafiri wa uhakika pasipo kupata unyanyasaji wowote ambao unaweza kufanya achukie shule kutokana na adha ya usafiri.

Amesema mabasi yaliyopo na mahitaji ya abiria hayatoshi wataendelea kuongeza ili wananchi kuwa na uhakika wa safari zao na kuweza kuleta maendeleo ya nchi.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad