Kampuni ya Simu Tanzania (TTCL) imeendelea kutoa dozi kali kwa timu inazokutana nazo katika Mashindano yanayoshirikisha timu kutoka Taasisi za Umma, baada ya mwisho wa wiki iliyopita kuifunga Banki Kuu ya Tanzania (BOT) kwa goli 1-0.
Goli la ushindi la TTCL limefungwa na mshambuliaji hatari Juma Masudi, kwa matokeo hayo, TTCL inashika nafasi ya pili katika msimamo wa Kundi B ikiwa nyuma mchezo mmoja dhidi ya kinara wa kundi hilo BOT.
Kikosi cha timu ya TTCL kilichocheza dhidi ya BOT, Kiwanja cha TPDC mwisho wa wiki iliyopita
Kikosi cha timu ya BOT kilichocheza dhidi ya TTCL, Kiwanja cha TPDC mwisho wa wiki iliyopita
Wachezaji wa TTCL wakipeana mikono na wachezaji wa BOT kabla ya mechi kuanza, Kiwanja cha TPDC mwisho wa wiki iliyopita
No comments:
Post a Comment