HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Friday, December 30, 2016

FRANCIS CHEKA AMFATA PROMOTA KAIKE DAR

Na Humphrey Shao

Bondia wa ngumi za kulipwa nchini mwenye makazi yake Mkoani Morogoro ameondoka mjini humo kwenda Dar es Salaam kuitikia wito wa Polisi.

Cheka ambaye alijisalimisha katika kituo cha Polisi Morogoro baada ya kupokea wito wa kufika kituoni kufuatia kupata barua ya wito huo.
  
"Nimefika kituoni na kuelezwa kuwa nimefunguliwa mashtaka ya kujipatia fedha kwa njia ya udanganyifu kutoka kwa Promota Siraju Kaike  hivyo nimefika hapo na kujidhamini na kuamua kwenda kituo cha Polisi Osterbay kwa ajili ya kutoa maelezo" amesema Cheka.

Amesema kuwa mashabiki wake wawe na imani nae kwani huo sio utapeli kama unavyozungumzwa bali ni mapromota uchwara wanataka kula migongoni mwa mabondia.

"Lazima nikwambie ndugu mwandishi Mimi nishakuwa mkubwa sasa na hizi ngumi zinauma hivyo Biashara ya pesa baadae ilishapitwa na wakati" alisema Chema.

Hivyo tuombe mungu mambo yote yatajulikana mahakamani.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad