HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Thursday, December 1, 2016

BODI YA WADHAMINI SIMBA KUTOA TAMKO KESHO


Mwenyekiti wa bodi ya wadhamini Simba, Hamisi Kilomoni (pichani)

KUELEKEA Mkutano mkuu wa dharula uliotishwa na Kamati ya Utendaji ya Simba ikiongozwa na Rais Evance Aveva, bodi ya wadhamini wa timu hiyo imeamua kujitokeza hadharani na kuongelea mikakati ya timu yao kuelekea duru la pili la Ligi Kuu Vodacom Desemba 17.

Bodi hiyo, ikiongozwa na Mwenyekiti Mzee Hamisi Kilomoni, itazungumza na waandishi wa habari na kuelezea mikakati yao ya kuhakikisha timu hiyo inaendelea kufanya vizuri pamoja na kuwaeleza wanachama wa timu hiyo masuala mazima ya timu yao.

Mkutano huo unaotarajiwa kuwa kesho, unaweza kuwa pia ni msumari kwa uongozi wa Simba kuelekea mkutano mkuu kwani Mzee Kilomoni amesema kuwa wao kama bodi ya wadhamini hawana taarifa yoyote ya mkutano huo.


No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad