BAADA ya kushindwa kufurukuta mbele ya Mbeya City benchi la ufundi la Yanga limemshushia lawama mwamuzi wa mchezo huo Mrope Rajab kuwa aliwaumiza katika kufanya maamuzi yake kwenye mchezo huo uliomalizika kwa Yanga kufungwa 2-1.
Kocha msaidizi wa Yanga Juma Mwambusi amesema kuwa ni kweli wachezaji wake waliteleza lakini refa wa mchezo huo amewaumiza kwa maamuzi yake yake aliyoyafanya kwa kuruhusu wachezaji wa Mbeya City kupiga mpira wa adhabu kabla wachezaji hawajamaliza kujipanga.
"mwamuzi ametuumiza kwa kufanya maamuzi ambayo yaliwatoa mchezoni wachezaji wake na kilipelekea kusababisha vurugu kwa kutoa maamuzi yanayotatanisha ,"amesema Mwambusi.
Mwambusi amesema tumeteleza na refa ametuumiza kwani aliombwa apime hatua ili kuweza pigo la adhabu kupigwa na akakubali lakini wachezaji wa Mbeya City wakaanzisha mpira wakati golikipa bado akiwa anapanga wachezaji.
Kutokana na tukio hilo ilibidi benchi la ufundi wawatulize wachezaji ambapo tayari wakatoka mchezoni na morali na kwanii goli la kwanza hawakulikataa iweje la pili waumie sana.
No comments:
Post a Comment