HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Tuesday, November 29, 2016

TIMU YA CHAPECOENSE YAPEWA HESHMA YA UBINGWA WA COPA SEDAMERICANA.


 WACHEZAJI wa timu ya Chapecoense waliopanda Ndege iliyokuwa safarini kutoka Bolivia imepata ajali Nchini Colombia leo majira ya saa mbili asubuhi kwa saa za Afrika Mashariki walipokuwa walisafiri kwenda kwenye mchezo wao wa fainali ya Copa Sudamericana, dhidi ya timu ya Medellin, Atletico Nacional.

Mechi ya awamu ya kwanza ya kombe hilo, la pili kwa umuhimu Amerika Kusini, ilikuwa imepangiwa kuchezwa Jumatano lakini sasa imesitishwa.

Atletico Nacional ambapo ndio wangekuwa wenyeji wa mchezo huo wa fainali ya kwanza, wameomba shirikisho la soka la America Kusini (CONMEBOL) kuwa kutoa Kombe hilo kwa timu ya Chapecoense ya Brazil kama sehemu ya heshima

Timu hito inayotoka mji wa Chapeco, kusini mwa Brazil, ilipandishwa kucheza ligi ya daraja ya kwanza nchini Brazil mwaka 2014 na ilifika fainali ya kombe hilo la Sudamericana kwa kulaza San Lorenzo ya Argentina.

Klabu ya Chapecoense Ilianzishwa 1973 ikapandishwa kucheza ligi ya daraja ya kwanza Brazilian, Serie A, mara ya kwanza 2014. Kwa sasa ipo nafasi ya tisa katika msimamo wa ligi.

Walikuwa wanaelekea kucheza fainali ya Copa Sudamericana, mshindi hufuzu kucheza Copa Libertadores, shindano kubwa la klabu Amerika Kusini. Na Jiji lao la nyumbani ni Chapeco katika jimbo la Santa Catarina, Brazil

Jitihada za maofisa uokoaji wa nchini Colombia limefanikiwa kufika eneo la tukio lakini waliopatikana hai ni watano na wachezaji wote kupoteza maisha.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad