HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Wednesday, November 30, 2016

NAIBU WAZIRI MAMBO YA NJE ATEMBELEA UBALOZI WA TANZANIA NCHINI KENYA

Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Susan Kolimba, ambaye yuko Nairobi kuhudhuria kikao cha Bunge la Afrika Mashariki, ametumia fursa hiyo kutembelea Ubalozi wa Tanzania nchini Kenya na kuzungumza na watumishi.


Katika kikao na Mhe. Waziri, watumishi wa Ubalozi walielezea changamoto mbalimbali wanazokabiliana nazo katika utendaji wa kazi, ikiwa ni pamoja na ufinyu wa bajeti. Hata hivyo watumishi hao walisema wameweza kukusanya maduhuli ya kuridhisha na kuhudumia Watanzania wanaopatwa na matatizo kwa kuchangishana wakati mwingine.

Mhe. Kolimba alieleza kuridhishwa kwake na utendaji wa watumishi wa Ubalozi wa Nairobi na kuwapongeza kwa moyo wa kujitolea. Alisema Serikali itajitahidi kupatia balozi fedha na vifaa vya kazi kwa kadri ya uwezo wake, lakini akasisitiza watumishi wawe wabunifu na wajitolee kufidia pale upungufu unapojitokeza.

Kikao cha Bunge la Afrika Mashariki kinachofanyika kwenye Bunge la Kenya kinatarajiwa kumalizika kesho.
Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Susan Kolimba (kushoto) akifurahia bidhaa za Tanzania kwenye ofisi za Ubalozi Tanzania jijini Nairobi akiwa na Kaimu Balozi, Bi. Talha Mohamed Waziri.
Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Susan Kolimba akiongea na watumishi wa Ubalozi. Kushoto ni Kaimu Balozi, Bi. Talha Mohamed Waziri na Mkurugenzi wa Sera na Mipango wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Bw. James Lugaganya. 
 
Baadhi ya watumishi wa Ubalozi wakijipanga kumpokea Mhe. Naibu Waziri
 
Mhe. Kolimba akisalimiana na baadhi ya watumishi wa Ubalozi.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad